Spika wa Bunge la Oman pamoja na wabunge 6 na wafanyakazi wengine wa Bunge la Oman, (Majlis A'shura) Sheikh Khalid Bin Bilal Bin Nasir Al Maawali leo ametembelea mbuga la wanyama na kushuhudia sehemu ya 'Great Migration' katika mbuga la Serengeti. Spika huyo ameishauri Tanzania kuitangaza zaidi utalii kwa kupitia vyombo vyote vya habari pamoja na mitandao ya kijamii ili kuvutia watalii wenye uwezo wa kifedha zaidi. Amehaidi ushirikiano wa kuitangaza Tanzania katika Inchi ya Oman na kuifanya iwe kivutio kwa wawekezaji wa kiarabu zaidi.
Spika wa Bunge la Oman, (Majlis A'shura) Sheikh Khalid Bin Bilal Bin Nasir Al Maawali na msafara wake wakishuhudia The Great Migration katika mbuga ya wanyama ya Serengeti leo
Msafara wa Spika wa Bunge la Oman, (Majlis A'shura) Sheikh Khalid Bin Bilal Bin Nasir Al Maawali
Nyumbu kila mahali Serengeti
Msafara ukikata mbuga
Mapumziko ya muda
Spika wa Bunge la Oman, (Majlis A'shura) Sheikh Khalid Bin Bilal Bin Nasir Al Maawali akisema machache kuhusu umuhimu wa kuitangaza Serengeti kimataifa
Spika wa Bunge la Oman, (Majlis A'shura) Sheikh Khalid Bin Bilal Bin Nasir Al Maawali na ujumbe wake pamoja na wenyeji wake.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...