Mmoja wa watoto wanaendelea na matibabu Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam, akiwa bize na rangi wakati walipotembelewa na mchora katuni Nathan Mpangala kupitia mradi wake wa kujitolea wa Wafanye Watabasamu, Jumamosi iliyopita. Mradi huo unaoshirikisha ndugu, jamaa, marafiki na wachoraji wenzake, ulikwenda kuwafariji kwa kuwapa zawadi kisha kuchora nao.
Mratibu wa mradi wa kujitolea wa Wafanye Watabasamu, Katunisti Nathan Mpangala ‘Mtukwao’, akishea jambo na mmoja wa malaika Hospitali ya Taifa Muhimbili, upande wa saratani, Jumammosi iliyopita.
Marafiki wa Wafanye Watabasamu, walionesha tabasamu mapemaaaaa.
Sanaa inamchango mkubwa katika kupunguza msongo wa mawazo na kusahaulisha maumivu.
Mchora vibonzo wa ITV ambaye pia ni mratibu wa Wafanye Watabasamu, Nathan Mpangala akiwa na mchora vibonzo wa baadae.
NYUMBA TU, SIMPO. Akiendelezwa atakuja kuwa mchoraji mahiri wa majengo.
Mchoraji katuni wa gazeti la Nipashe, Abdul King O aka ‘Kaboka mchizi’, aliungana na Wafanye Watabasamu kuwatabasamisha malaika hawa. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. Mungu akubariki Nathan na wote mlioshiriki.

    ReplyDelete
  2. Nathan, ndugu na marafiki zako Mungu awabariki kwa kazi nzuri ya kujitolea. Big up sana sana

    ReplyDelete
  3. Abdul King O,tuttafutane bhana japo kwa salaam tumepoteana sana

    Bard Mkoba wa mchikichini
    0655566555

    ReplyDelete
  4. Good work Nathan Mpangala, I am impressed with this.

    ReplyDelete
  5. Mungu awazidishie Nathan na wote mlioshiriki kuwatembelea malaika hawa.

    ReplyDelete
  6. Hivi mafisadi yenye mabillions hayana hata aibu, hizo hela walizotuibia zingekuwa zinawsaidia hawa watoto.

    ReplyDelete
  7. "Artist must be true" Nathan you proved it. mungu akuzidishie na akupe ubunifu zaidi wa kuifanya jamii yako iendelee kutabasamu

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...