TAHADHARI:- KUNA TAPELI MWENYE ASILI YA KIZUNGU ANADAI YEYE NI RAIA WA AFRICA KUSINI. Ni MREFU, ANAONEKANA SANA MITAA YA KINONDONI KWA MANYANYA JIJINI DAR MIDA YA USIKU. AMETAPELI WATU WENGI SANA AKIDAI KUA AMEIBIWA HOTELINI NA MWANAMKE NA ANADAI ANAISHI MBEZI KIMARA. KWA WENYEJI WENGI WA KINONDONI WANAMFAHAMU NA WENGI WAMESHAMSIKIA NA WANADAI NI MSWAHILI. CHUKUENI TAHADHARI NA TUKO KWENYE HARAKATI ZA KUMKAMATA KWA SABABU AMESHA TAPELI WENGI AKIJIFANYA KUCHUKUA NAMBA ZA SIMU KWA AJILI YA KUREJESHA FEDHA HIZO TUNAOMBA WENYE TARIFAA ZAIDI WATUSAIDIE KWA USHIRIKIANO NA POLISI KUMTIA MBARONI IMETOLEWA NA MMOJA YA WALIOLIZWA |
Home
Unlabelled
TAPELI WA KIZUNGU ANASAKWA:-TAARIFAA KWA VYOMBO VYA HABARI NA UMMA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
TIT FOR TAT...No Complain please, Mmewaliza sana wathungu, Nao sasa zamu yao! ahahaha... This is Africa Bwana. kuna vihoja hadi Raha, Naipenda Afrika. Yani am so happy nilizaliwa mwafrika. poleni mliopigwa na mthungu, hehehe Bongoooo!!Safi sana. Tafuteni ule mwimbo wa Professor Jay, Bongo Dali salamu. Aliyaona haya akayaimba. LOLZ
ReplyDeleteHakuna Mzungu aliyekuwa sio tapeli. Hata kama ni Profesa. Jihadhari na Wazungu. Mzungu yeyote anaishi kwa leo. Atafanya chochote ili afikie lengo hilo. Kama kutapeli kutamfanya aishi basi atatapeli.
ReplyDeleteMdau
UK
Weee huo ndio ujinga wetu, sasa unampatia pesa mtu ambaye humjui au kwa vile Mzungu!! Ajabu, wala huna haja ya kutangaza acha azitafune hizo pesa hamna kazi nazo
ReplyDeleteHuyo Tapeli amekuwepo muda mrefu (ama mzungu mwingine tapeli kama siyo yeye). Alikwishaniliza Mikocheni. Alijitambulisha kuwa American japo accent si American. Nilimwamini kwa vile si Waamerika wote wana American accent. Anaomba pesa kuwa ameibiwa na amekwama hotelini. Anatembea sana kwa mguu. Na anakuwa ametoka jasho sana. Lakini kwa vile anaomba watu wengi kwa siku huwa hawakumbuki sura anazoomba. Baada ya kunitapeli Mikocheni, siku nyingine akanisimamisha mjini na story ile ile. Nikamwambia kuwa nilikwishamsaidia huko nyuma kwa hadithi hiyo hiyo. Akaona aibu akaondoka. Lakini kabla ya hapo nilikuwa nimekwishamwona kwa mbali akisimamisha watu wengine pia na kuwatapeli. Siku moja akanisimamisha tena Kijitonyama na kutoa hadithi hiyo hiyo. Siku hiyo nikamuitia polisi (CID) kwa simu. Polisi alipokuja akaongea nae halafu akamwachia. Kwa hiyo polisi hakuna msaada juu ya hili. Ni wananchi wenyewe tu wajihadhari.
ReplyDelete
ReplyDeletewe mpuuzi hapo juu kwani na walio walipo tugeuza slaves na kutufanya kama properties unadhani ilikua haki?? tena waacha wazidi kulizwa huyo mzungu anatakiwa kuchomwa moto
HAAA KWENI NI HUYO TU MBONA WAKO WENGI NA WALE WALIOKUWA WAKITAPELI NA KINA PAPAA MSOFI NA MZAMIRU TENA MAMILLION YA MAPESA MBONA HASEMI? HUYO MZUNGU NI MSELA HANA SEHEMU YA KULALA NDIO MAANA ANAKWENDA HOVYO KWENYE MABAA KINONDONI AKIKOSA KULIPUA ANALALA KWA MACHANGUDOA, MIMI NAMJUA HANA UHALIFU HUO ANAKUOMBA UKIMPA SAWA UKINYIMA HATUMII NGUVU . MAISHA HAYO!
ReplyDeleteNdio mkome maana kuna mijitu ikishamuona hiyo mizungu basi chochote anacho mwambia linakubali pasipo kufikili mijinga sn nyie mnaolizwa.
ReplyDeleteHahahahahah!!!
ReplyDeleteMdau wa kwanza mara zote ''Mla kunde huwa rahisi kusahau lakini Mtupa maganda hawezi kusahau''
Wa-west Afrika na Watanzania wamesha fanya Maafa makubwa sana Ulaya na Marekani.
Na sasa Wazungu nao wanalipiza Kisasi.
Tukumbuke ya kuwa Mwosha huoshwa!
Ebwana eee!
ReplyDeleteSisi upigaji wetu ulikuwa ni ule ule wa kuunga unga na labda kwa Msaada wa HIRIZI na TUNGULI kidogo!
Duuu 'Mibao ya Kupigwa' kwa kulipiziwa Kisasi ya Wazungu mbona tutakoma?
Sasa Mzungu mwenye kila kitu ktk Sayansi na Tekinolojia HUKU AKIWA ANAAMINIKA KIRAHISI SANA KULIKO SISI si ndio tutafikia Kupigwa na Wazungu hadi kuuzwa kama Ng'ombe na Bata?
Hili ni JEMBE ULAYA Kiboko yao!!!
ReplyDeleteTena Mzungu Nampa Assalam Aleko zake kwa kuianzia Operesheni yake kule kule kulikoungua Mpini na jembe likabaki KINONDONI kwenye Makao Mkuu ya Wasanii wa Mjini.
Ninyi Kinondoni si ndio mnao jiita na kujifanya Watoto wa Mjini? mie akuu nakaa kwetu Mbagala nimekomboka, vipi tena mnalalamika kugandamizwa nao?
Jembe Ulaya !
Ohooo !
ReplyDeleteHodi hodi Yanga S.C wana Jangwani, mmeona Shabiki wenu KIVULI, NYATU NYATU huyo anajipanga?.
Mmeona Flana aliyovaa?, ina Rangi za Yanga na alama ya Afrika ya Yanga!!!
Baada ya Kinondoni MZUNGU akishawacharaza anakuja Klabuni Yanga!!!
Akifika atafanya hivi:
1.Ataghushi Hati za Jengo la Klabu.
2.Ataghushi Mikataba ya wachezaji wooote na Makocha.
3.Ataghushi ktk Nyaraka za Vikao na kujiweka kama Raisi wa Klabu.
BAADA YA HATU HIZO 3 HAPO JUU ATAIUZA KLABU YA YANGA KWA NCHI ZA NJE ATAKOMBA FEDHA KWA KULIPWA KTK AKAUNTI YAKE HUKO KWAO KWA NJIA YA MTANDAO.
HALAFU ATATOROKA KWENDA NCHI YEYOTE KWA KUWA YEYE HAOMBI VISA KAMA MARAISI WA KLABU ZA YANGA NA SIMBA KAMA AKINA LLOYD NCHUNGA NA ESMAEL ADEN RAGE, MZUNGU HUYOOO ATAHAMIA VISIWANI KULA BATA!
Na huyu jamaa kichwa cha nazi kweli.Hugh mzungu ana ikichwa?wacha kuwa mshamba
ReplyDeletehuyo jamaa ndio kwaidayake sio mzungu kweli nimzungu warang ,anakaa kinondoni kwamanyanya mtaa furani hunainyeshwa mpira hapo sehemu kumeandikwa chelsea anaitwa john mama yake nimzungu nz babaya mswahili mama yake mwalimu mkuu washule anayomiliki baba yake wakambo na huyo babayake wakamba ni dr mstaafu pia nimteja wa kuvuta unga kama hujui anajifanya kuongea kingereza
ReplyDeleteHenhe henhe hen!
ReplyDeleteMzungu ametumia akili ameunda hadi Madege, Mitambo na Magari halafu leo anakuja zidiwa akili na Mtanzania na kwa kwa miaka mingi tu amekuwa akitapeliwa na akilizwa?
Ndio amaana jamaa Mzungu akaona aje Tanzania kuja kujibu mapigo!
Kinondoni mmemuona 'Kinyozi' wenu wa Kizungu huyo?
ReplyDeleteOhhh Mzungu ameona aanzie Kinondoni KUWAPIGA MIKWAJU kwa kuwa ndio kuna idadi kubwa sana ya Wasanii wa Mujini!!!
Kinondoni mwaka huu na Usanii wenu mtakoma!
ReplyDeleteMzungu atawa bonyeza na kuwagandamiza zaidi KIDIJITALI !
Tukumbuke hapo ni Kinondoni 'Shamba la Tanzania' hapo ni Brazil ya Tanzania.
ReplyDeleteMzungu huyo atakuwa TEJA!
Kikubwa kinacho tugharimu Watanzania Wakonongo ni kuwaamini sana na kuwapa nafasi Wageni hasa watu weupe.
ReplyDeleteAngalieni leo hii haya yanajiri Tanzania pekee dunia nzima hakuna nchi inayotoa ubwete kwa wageni kama Bongo.
1.Mabenki yanatoa Fedha kirahisi sana kwa Wageni hasa weupe.
2.Idara za Mamlaka zipo legevu sana kwa wageni hasa weupe.
3.Ktk jamii zetu mitaani Wageni hasa weupe wanaaminika sana na kirahisi rahisi.
Nakwambia kwa Mtaji huo hapo juu (hayo matatu 3) hapa wataliwa wengi sana!
Kutokana na Kinondoni kukomaa kwenu Kiusanii Mzungu ameonelea aje kuwachapa nao awamwage kinyesi na kuzaa na ninyi !
ReplyDeleteJamaa atawa fanyia Usanii hadi mkome.
Mtazaa na Mzungu !