Jumamosi ya tarehe 29 March 2014, watanzania waishio na wasomao Malaysia walikutana katika Ubalozi wa Tanzania na kuunda Jumuiya mpya ya Watanzania wanaoishi South East Asia.

Uongozi wa Wana Jumuiya hiyo ambao kwa kuanzia ni Watanzania waliopo Malaysia wakiwa na Balozi Mpya wa Tanzania,Dr. Aziz Ponary Mlima (katikati) na maafisa wa Ubalozi. Viongozi waliochaguliwa ni Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Katibu Mkuu, Waziri wa Fedha, Waziri wa Elimu, Waziri wa Jamiii, Utamaduni na Starehe ikiwa pamoja na Wadhamini wawili.

Picha nyingine ni Watanzania wote kwa pamoja na wafanyakazi wa Ubalozi na Balozi Mpya wa Tanzania nchini Malaysia.

Jumuiya hiyo ilianzishwa Mwishoni mwa wiki,ambayo inajulikana kama " Tanzanian Diaspora in South East Asia" ambayo itakuwa inawashirikisha Watanzania wote katika nchi za Malaysia, Indonesia, Thailand, Philippines, Brunei, Laos na Cambodia.

Picha zaidi zinaweza kuonekana kwenye Ukurasa wa Facebook


Watanzania kutoka maeneo hayo wanaombwa kujiunga ili tuweze kutambuana na itakapokuwa lazima kusaidiana.

Kwa niaba ya Tanzanian Diaspora South East Asia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...