Wananchi wa kijiji cha Naiyobi wilaya ya Ngorongoro
wakichota maji
ambayo hutumia na mifugo kijiji hicho kinakabiliwa na uhaba wa
maji
Na Woinde
Shizza,Arusha
WANANCHI wa
Kijiji cha Nayobi kilichopo tarafa ya Ngorongoro
wilayani
Ngorongoro mkoani Arusha wamelalamikia kero ya uhaba wa
maji
inayowasababishia kukesha kwenye bomba la kijiji kwa takribani siku
tatu
wakisubiri maji jambo linalopelekea shughuli za kijamii na
kiuchumi
kusimama kwa muda mrefu na kinamama kutembea umbali mrefu wakitafuta
huduma hiyo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi hao wamesema kuwa kwa muda
mrefu wamekua wakiteseka kupata huduma za maji huku kinamama
wajawazito wakijifungulia bombani apo baada ya kukaa kwa muda wakitafuta maji
huku wengine wakilazimika kukesha na watoto wadogo.
Wanakijiji Daniel Sereki na Rehema Laizer na
wamesema kuwa kwa sasa
wanakabiliwa na tatizo kubwa la uhaba wa maji pamoja na chakula na
hata
pale wanapopata chakula hukosa maji ya kupikia chakula hicho na
kuziacha
familia zao zikitaabika kwa njaa.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji Naiyobi Meleji Sikoni
amesema kuwa kwa muda wa miaka 20 wamekua wakikabiliwa na tatizo la uhaba wa maji
hivyo ameiomba serikali na mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro iwasaidie
kutatua tatizo hilo sugu linalowaathiri wananchi wengi.
Mgombea Ubunge Jimbo la Ngorongoro Wiliam Olenasha ameeeleza
kisikitishwa na wananchi wanaoteseka kwa kero ya maji ambayo hushirikiana na
mifugo katika matumizi yake hivyo ameaidi kutatua kero hiyo pindi
atakapopata ridhaa ya kuongoza wilaya hiyo.
Wilaya ya Ngorongoro inakabiliwa na changamoto ya uhaba wa maji pamoja
na chakula hasa katika kipindi hiki cha kiangazi ,juhudi zinahitajika
kwa upande wa serikali na Mamlaka ya Ngorongoro ili kuweza kuwanusuru
wananchi na baa la njaa pamoja na uhaba wa maji.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...