Na. Tamimu Adam- Jeshi la Polisi
Jeshi la polisi nchini limewataka wananchi kuimarisha na kutekeleza kwa vitendo dhana ya ulinzi jirani katika kipindi hiki cha kuelekea kuadhimisha sikukuu za mwisho wa mwaka na kusherekea mwaka mpya kwani ulinzi jirani ni mkakati madhubuti katika kuimarisha usalama wa raia na mali zao hapa nchini.
Hayo yalisemwa na Msemaji wa Jeshi la Polisi, Mrakibu mwandamizi wa Polisi Advera Bulimba wakati akitoa tahadhari ya usalama katika kipindi hiki cha kuelekea mwisho wa mwaka, ofisini kwake makao makuu ya Jeshi la Polisi, jijini Dar es salaam.
“Uzoefu unaonyesha kuwa kipindi cha kuelekea mwisho wa mwaka na hususani sikukuu za mwisho wa mwaka baadhi ya watu hupenda kutumia fursa hiyo kujipatia kipato kwa njia isiyo halali kwa kufanya udanganyifu, wizi na utapeli katika maeneo mbalimbali hivyo wananchi wanatakiwa kuwa macho katika shughuli zao” Bulimba alisema.
Aliongeza kuwa Jeshi la Polisi nchini limejipanga kikamilifu kwa kufanya doria katika maeneo yote kuhakikisha wananchi wanasheherekea na kumaliza mwaka kwa amani na usalama pasipo hofu yoyote yakufanyiwa vitendo vya uhalifu.
Aidha, aliwataka wafanyabiashara na wamiliki wa hoteli hapa nchini kuweka kamera na vifaa maalumu vyenye uwezo wa kufuatilia mienendo ya watu wanaoingia na kutoka katika maeneo yao ya biashara ili kuweza kuwabaini wahalifu na uhalifu kwa haraka.
Pia alitoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi wanapowatiria shaka watu wasiowafahamu katika maeneo yao kwa kutoa taarifa kwa namba za bure ambazo ni 111 na 112, namba hizi ni za dhalura na ukipiga katika mkoa wowote ulipo zitapokelewa na hatua za haraka zitachukuliwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...