Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa JOWIKA KASUNGA amewataka waalimu Wilayani Mufindi kujiepusha na masuala ya ulevi, uwasherati sanjari na maneno ya ovyo ili wawe mfano bora kwa wanafunzi wanaowafundisha kwa shabaha ya kuimarisha nidham jambo ambalo litachangia kuongeza ufaulu wilani humo.

Taarifa ya Ofisi ya habari na mwasiliano kwa umma ya Halmashauri ya wilaya ya Mufindi kwa vyombo vya habari, imebainisha kuwa, Mkuu huyo wa Wlaya ameyasema hayo kwenye kikao maalum cha tadhimini na kutunuku zawadi kwa shule zilizofanya vizuri zaidi kwenye mitihani ya kumaliza elimu ya msingi iliyofanyika mapema mwaka jana ambapo Wilaya ya Mufindi ilipanda kwa aslimia 11 na kushika nafasi ya pili Kimkoa.

Kasunga ambaye pia ni mwalimu kitaaluma ameongeza kuwa, waalimu wanawajibu wa kulinda hadhi ya uwalimu katika jamii na kuacha vitendo vinavyo dhalilisha tasnia yao kisha akasisitiza kuwa taaluma ya uwalimu itabaki kuwa wito na kufafanua kuwa dhana ya uwalimu ni kama kazi nyingine ituike tu wakati wa kudai maslai bora ya walimu na si kuilinganisha na taaluma nyingine.

Kwa pande wao baadhi ya waalimu wakuu wa shule za msingi zilizofanya vizuri zaidi na kupandisha ufaulu kutoka aslimia 68. 2 mwaka 2014 mpaka asilimia 80. 3-9 mwalimu JACKSON MKOLA wa shule ya msingi HOLO na Mwalimu EVER MWANJESI shule ya msingi Mjimwema wamesema ushirikiano na na kufanya kazi kwa kujituma ndio chachu ya mafanikio hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...