SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) inapenda kuwakumbusha wanafamilia wa mpira wa miguu kuto kushiriki katika michezo ya kubahatisha (Betting)juu ya ibara ya 59 kifungu kidogo cha 11 kinachotamka:
TFF Family members shall at all times comply with the following ethical principles "To not take part in betting connected with football and do not tolerate any form of manipulation or unlawful influencing of match results".
Hivyo wanafamilia ya mpira wa miguu Tanzania wanakumbushwa kuheshimu Katiba ya TFF Kwa kutoshiriki katika michezo ya kubahatisha (betting).
Wanafamilia ya TFF ni pamoja na viongozi wa mpira wa ngazi, zote, wachezaji, makocha, waamuzi, makamisaa, waajiriwa wa TFF, wajumbe wa kamati mbali mbali za TFF na wengine wote ambao kwa namna moja au nyingine wanajihusisha na mpira wa miguu
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...