1
Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu Balozi Ombeni Sefue akizungumza na Menejimenti ya Wakala wa Taifa wa Utafiti wa Nyumba Bora na Vifaa vya Ujenzi na Vifaa vya Ujenzi (NHBRA) wakati alipofanya ziara katika taasisi hiyo mwishoni mwa wiki ili kujionea shughuli mbali mbali zinazofanywa na taasisi hiyo , Kwa kiwango kikubwa (NHBRA) imeonyesha ni taasisi inayoweza kujenga nyumba za bei nafuu sana hasa vijijini ili watanzania wa maeneo hayo waweze kupata makazi bora ya kuishi kwa bei rahisi zaidi, Kulia katika picha ni Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo Bw.Matiko Samson Mturi.
Taasisi hiyo pia imekuwa ikijihusisha na mafunzo teknolojia ya ujenzi wa nyumba za bei nafuu kwa vikundi mbalimbali nchini ikiwa ni pamoja na kuwafundisha juu ya utengenezaji wa matofali, vigae vya kuezekea nyumba pamoja na ujenzi wa nyumba za zenyewe ambapo taasisi na wananchi mbalimbali wanaweza kufaidika na mpango huo nchini.2Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo Bw.Matiko Samson Mturi akizungmza wakati alipokuwa akimkaribisha Balozi Ombeni Sefue wakati alipotembelea katika taasisi ya Wakala wa Taifa wa Utafiti wa Nyumba na Vifaa vya Ujenzi NHBRA Mwenge jijini Dar es salaam.
3Bw. Sylivester Shumbusho Fundi kutoka Wakala wa Taifa wa Utafiti wa Nyumba na Vifaa vya Ujenzi NHBRA akimpa maelezo Balozi Ombeni Sefue juu ya utengenezaji wa matofali ya bei rahisi kwa kutumia udongo wakati alipokuwa akitembelea karakana ya taasisi hiyo iliyopo Mwenge jijini Dar es salaamKatikati ni Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Bw. Matiko Samson Mturi.
4Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Bw. Matiko Samson Mturi akimpa maelezo Balozi Ombeni Sefue wakati alipokuwa akitembelea na kukagua shughuli mbalimbali katika taasisi hiyo kulia ni Bw. Sylvester Shumbusho Fundi katika taasisi hiyo.
6
Baadhi ya wafanyakazi wakiendelea na shughuli za kutengeneza vigae vya kuezekea nyumba katika karakana ya taasisi hiyo.
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...