Na Is-haka Omar, Zanzibar.

CHAMA cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimewataka wananchi wanaoishi katika maeneo yanayomilikiwa na chama hicho kuhakikisha wanafunga mikataba rasmi ili kuepuka usumbufu wakati maeneo hayo yatakapohitajika kwa ajili ya shughuli za kichama.

Kimesema kuna baadhi ya wananchi waliopewa maeneo ya kuishi kwa muda kwa nia ya kuwasaidia na badala yake wameyageuza kuwa makaazi yao ya kudumu jambo ambalo sio sahihi.Akizungumza Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Ndg. Vuai Ali Vuai kwa nyakati tofauti katika mwendelezo wa ziara ya kuhakiki mali na maeneo mbali mbali yanayomilikiwa na CCM huko Mbweni Mkoa wa Magharibi Kichama.

Alisema chama kinaendelea na zoezi la kuhakiki mali zake kutokana na kuongezeka kwa vitendo vya udanganyifu vinavyofanywa na baadhi ya watu wasiokuwa waaminifu wanaotengeneza hati na mikataba bandia ya kujimilikisha mali za chama hicho kinyume na utaratibu.

Ndg. Vuai alifafanua kwamba katika hatua za kupunguza kero hizo chama kimeamua watu wote ambao wamepewa kibinadamu sehemu za kuishi ama kufanya biashara kwa muda katika maeneo yanayomilikiwa na CCM wafunge mikataba rasmi ili chama kiweze kunufaika na rasilimali zake.

“ Watu waliopewa kwa dharura sehemu za kuishi na kufanya biashara kama hatujawapa mikataba rasmi inayotambulikana kisheria, ambayo ni kielelezo cha kumtambulisha nani mmiliki halali wa maeneo hayo baadae inaweza kuwa fursa ya kufanya utapele na kusababisha usumbufu na lawama kwa chama. 

Tujaalie kwamba mtu anaishi katika kiwanja cha Chama bila mkataba wa kisheria na imetokea ameondoka au amehama watoto, ndugu na jamaa zake hawatokubali mali hizo zirudishwe kwa CCM na kitakachotokea hapo ni ugomvi na kupelekana mahakamani hali ambayo chama hakipo tayari kuona inatokea ”,. Alifafanua Vuai na kuongeza kuwa CCM haitokuwa tayari kuona mali zake zinatumiwa na watu wachache bila ya makubaliano ya kimaandishi ama mikataba ya kisheria.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...