Na. Mwandishi wetu, Bahi

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto, Ummy Mwalimu amewahimiza wananchi wa wilaya ya Bahi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za afya.

Waziri Ummy alisema hayo leo wakati alipofanya ziara ya kikazi wilayani BAHI kwa kutembelea kituo cha Afya cha Mundemu.

Akijibu maswali ya wananchi kuhusu kutopewa dawa licha ya wao kuwa na kadi za CHF, Waziri Ummy amewahakikishia wananchi wote kuwa, wizara yake kupitia Bohari ya Dawa (MSD) itahakikisha dawa za kutosha zinapatikana kwenye vituo vya kutolea huduma ili wananchi na wanachama wa CHF waweze kupata dawa wakati wote."kupitia CHF iliyoboreshwa mtaweza kupata huduma hizo hadi ngazi ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa"alisema

Katika ziara hiyo,Waziri Ummy pia alitembelea mradi wa usafi wa mazingira mashuleni, katika jamii na maeneo ya kutolea huduma kwa jamii unaofadhiliwa na PLAN INTERNATIONAL .

Waziri wa afya akiongea na wagonjwa waliofika kituoni hapo kupata huduma.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akisalimiana na watumishi wa kituo hicho cha afya

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...