Pichani kati ni Mratibu wa tamasha la Dar Festival, Faridi Faradj akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani),jijini Dar es Salaam juu ya tamasha hilo litakalofanyika mwezi huu katika viwanja vya viwanja vya leaders club na siku ya pili ndani ya viwanja vya Makumbusho jijini Dar.Kulia ni Diwani wa Kata ya Ilala na kushoto ni mmoja wa Waratibu wa tamasha hilo, Shaban Kapilima.
Mratibu wa Tamasha hilo ,Faridi Faradj amesema kuwa tamasha jipya litalenga kutangaza na kudumisha utamaduni wa Tanzania,na kuwa tamasha hilo litahusisha michezo ya kiasili kama Bao,Karata itayoenda sambamba na burudani nyingine za ngoma za asili na maonesho ya baadhi ya tamaduni za makabila ya Tanzania.
" Pia tunategemea kuwa na mashindano ya kucheza ,vichekezo na maonyesho ya Muziki kutoka kwa baadhi ya Wasanii" alisema Faridi.
Amesema kuwa kutokana na utafiti inaonyesha watu wengi wamekuwa wakikosa matukio kama haya ya,hivyo wanatarajia tamasha hilo litapokelewa kwa furaha kubwa na Watanzania watajitokeza kwa wingi kwani litahusisha watu wa rika mbalimbali.
Akifafanua zaidi faida ya tamasha hilo,Faridi amesema kuwa tamasha hil litaendeleza umoja wa Watanzania,Burudani kwa Watanzania, kuwakumbusha Watanzania utamaduni wao, kutangaza utamaduni wa Watanzania samnbamba na kusaidia Serikali kupitia sekta ya utalii kuongeza mapato.
Faridi ametoa wito kwa wanahabari kulitangaza tamasha hilo ili wadau wajitokeza kwa kulidhamini,hivyo kwa pamoja watakuwa wamesaidia kudumisha utamaduni wetu na kuisaidia serikali yetu kutunza utalii.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...