Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Hamis Kigwangalla (kushoto) akipitia kwa makini jalada (file) la matibabu Bi. Kuluthumu Kasongo (aliyelala kitandani) anayesumbuliwa na ugonjwa wa Seli Mundu (Sicle Cell) kujiridhisha juu ya matibabu yake kufuatia taarifa zilizozagaa kwenye mitandao ya kijamii leo kuwa mgonjwa huyo ametelekezwa bila kupatiwa matibabu na kulazwa chini katika wodi hiyo jambo ambalo sio la kweli.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Hamis Kigwangalla (kushoto) akiwa ameongozana na Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mwananyamala Dk. Delila Moshi kufuatilia ziara yake ya kushtukiza aliyoifanya leo jijini Dar es salaam kuangalia ubora wa huduma za Afya zinazotolewa na hospitali hiyo.
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mwananyamala Dk. Delila Moshi (kulia) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Hamis Kigwangalla (kulia) juu ya huduma za Tiba alipotembelea wodi ya watoto njiti katika Hospitali ya Mwananyamala leo jijini Dar es salaam.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Hamis Kigwangalla (kulia) akizungumza na akina mama wenye watoto waliokuwa katika wodi ya Wazazi ya Hospitali ya Mwananyamala leo jijini Dar es salaam mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika hospitali hiyo.Amewahakikishia akina mama hao kuwa Serikali itaendelea kuboresha huduma za Afya katika hospitali zake.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Hamis Kigwangalla (kulia) akimsalimia mtoto aliyekuwa amelala na akina mama wenye watoto aliowakuta katika wodi ya Watoto Njiti katika Hospitali ya Mwananyamala leo jijini Dar es salaam mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika hospitali hiyo kukagua ubora wa huduma za Afya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...