Wasanii wa kikundi cha muziki cha Sauti Sol kutoka nchini Kenya wamefanya mahojiano na kituo cha redio cha Efm 93.7 fm kupitia kipindi cha Joto la Asubuhi kinachorushwa kila siku ya Jumatatu hadi Ijumaa kuanzia saa 12:00 hadi saa 3:00 Asubuhi.
KATIKA mahojiano hayo Sauti sol wamesema kuwa wanamuziki wa Afrika Mashariki wanalipwa vizuri katika show wanazozifanya ikilinganishwa na wasanii wa Nigeria, vilevile Lugha ya Kiswahili imekua Lugha nzuri yenye vionjo hivyo imeweza kuvutia wasanii wengi wa nje ya Tanzania kuitumia katika nyimbo zao.
Baada ya kufanya vizuri kwa nyimbo yao ya "Unconditional bae" walioshirikiana na msanii wa Tanzania Ali kiba, wamewataja pia wasanii wengine wa Tanzania ambao wanatarajia kushirikiana nao katika nyimbo zao zijazo ambao ni Vanessa Mdee, Weusi, pamoja na Diamond Platnumz.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...