Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa ameitaka Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA), kujenga chelezo (gereji ya kukarabati meli na vivuko), katika bandari ya Dar es Salaam ili kuokoa fedha nyingi zinazotumika kwa matengenezo nje ya nchi.

Waziri Prof. Mbarawa amesema hayo wilayani Kyela, wakati alipokuwa akikagua maendeleo ya ujenzi wa meli mbili mpya za mizigo zinazojengwa na Kampuni ya Songoro Marine katika bandari ya Itungi ambayo ni Bandari Kuu katika Ziwa Nyasa na kuelezea kuridhishwa kwake na hatua za ujenzi uliofikiwa.

“Tukijenga chelezo Dar es Salaam tutaokoa fedha nyingi tunazozipeleka nje kila mwaka kwa ajili ya ukarabati wa vivuko na meli zetu", amesema Waziri Prof. Mbarawa. Amesisitiza kuwa kujengwa kwa chelezo katika bandari hiyo kutaongeza ajira kwa wananchi na pato kwa mamlaka kwani vyombo vya Sekta binafsi vitaweza kufanyiwa ukarabati wa vyombo vyao vya majini.

Aidha katika hatua nyingine, Waziri Mbarawa amekagua mradi wa ujenzi wa barabara ya Kikusya-Ipinda- Matema KM 34.6 inayojengwa kwa kiwango cha lami na kumtaka Mkandarasi anayejenga barabara hiyo kukamilisha kwa viwango na ubora unaotakiwa ili idumu kwa muda mrefu.

"Tunapotoa fedha tumedhamiria kuhakikisha kitu tunachofanya kiendane na thamani ya fedha hiyo hivyo hakikisha unatekeleza kazi hii kwa kuzingatia viwango na ubora unaotakiwa",amesisitiza Prof.Mbarawa.

Hata hivyo Prof. Mbarawa amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa mkandarasi anayejenga barabara hiyo ili kuhakikisha kazi hiyo inakamilika kwa haraka na kufungua uchumi wa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.

Kwa upande wake Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) mkoa wa Mbeya Eng. Paul Lyakurwa amemuomba Waziri Mbarawa kuruhusu wahandisi wazalendo kuendelea kusimamia mradi huo ikiwa ni hatua ya kuwajengea uwezo watanzania kusimamia miradi mikubwa nchini.

Waziri Prof. Mbarawa yupo katika ziara ya kukagua miundombinu na kuongea na wafanyakazi waliopo chini ya wizara yake katika mkoa wa Mbeya.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akielekea katika Bandari ya Itungi kukagua maendeleo ya ujenzi wa meli mbili mpya zinazojengwa katika bandari hiyo wilayani Kyela.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Songoro Eng. Salehe Songoro akitoa maelezo ya hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa meli mbili mpya mbili kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, alipotembelea bandari ya Itungi kuona maendeleo ya ujenzi huo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akifafanua jambo kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Songoro Eng. Salehe Songoro wakati alipokagua moja ya mashine ya meli mpya inayojengwa katika bandari ya Itungi, wilayani Kyela.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (kushoto), akikagua risiti za malipo na Mhasibu wa Bandari ya Itungi (wa pili kushoto), wilayani Kyela.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...