Wahamiaji 21 waliokuwa wakivuka maji katika bahari ya Mediterranea ambao wazama na kupoteza maisha, wameripotiwa kuzikwa na wakazi wa mji wa Libya baada ya miili yao kukutwa ikielea ufukweni.
Mamlaka nchini humo zinasema zililazimika kuchukua hatua ya kuondoa maiti zilizokuwa zinazagaa ufukweni.
Miili hiyo ilikaa siku tatu katika pwani ya Al- Maya, kaskazini mwa Tripoli .
Wenyeji wa eneo hilo walijawa na hofu ya maiti hizo kusababisha magonjwa ndipo wakalazimika kuzizika.
Mohammed Garbaj ambaye amekuwa akijaribu kuwaokoa wahamiaji wanaozama. Chanzo: BBC SWAHILI.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...