Dotto Charles Heka (13) aliyekuwa Mwanafunzi wa shule ya msingi Lupungu wilayani Malinyi hatimaye amefufua ndoto zake za kuendelea na elimu ya sekondari.

Awali baada ya kuhitimu elimu ya msingi tu wazazi wake walimshinikiza na kumlazimisha aolewe pasipo yeye mwenyewe kuridhia kuishi na mtu mmoja aliyetambulika kwa jina la Masenga, kama mme na mke, akielezea kwa uchungu mbele ya Mkurugenzi wa wilaya ya Malinyi ndugu Marcelin Ndimbwa, Afisa elimu wa wilaya Kalagila Silivesta na mwanasheria Sospeter Kalekwa, mwanafunzi Doto Charles Heka anasema,kwakuwa hakupata kuungwa mkono na hata mmoja wa wazazi na ndugu zake alikubali kuoelewa hivyo hivyo. 

Baada ya matokeo kutoka baadhi ya wasamaria wema waligundua kwamba amefaulu na amechaguliwa kujiunga na shule ya sekondari ya kutwa ya Ngoheranga na kuamua kutoa taarifa wilayani iliyopelekea mkurugenzi kulivalia njuga jambo hilo na baada ya kujiridhisha aliweka mtego na jeshi la polisi lilifanikiwa kumkamata baba wa mtoto na kumchukua mtoto huyo ambaye mpaka sasa bado yupo chini ya uangalizi wake mkurugenzi na mtoto anaishi kwa mwalimu, akisubilia kufunguliwa kwa shule . 

Mbali na hayo yote pia Mkurugenzi ameamua kujitolea kumsomesha mwanafunzi huyo kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita na amemwomba afisa elimu mkoa amtafutie nafasi ya shule ya bweni huku Ndugu Masenga aliyetoroka akiendelea kutafutwa na jeshi la polisi na kuhakikisha anatiwa nguvuni na sheria kuchukua mkondo wake na kuwa onyo na somo kwa wengine wote wenye mawazo na tabia za namna hizo ndani ya halmashauri yake. Aidha mkurugenzi amewapongeza maafisa elimu, watumishi wa halmashauri hiyo pamoja na wasamaria wema waliotoa ushirikiano na kumnusuru binti huyo. Mungu atawalipa kwa haya mliyomtendea malaika wake Dotto.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...