Mpendwa Baba yetu Urban Peter Mbuya, leo umetimiza mwaka mmoja tangu mwenyezi Mungu akuite nyumbani kwake juu mbinguni. Umetuachia majonzi makubwa lakini tuna imani uko mahala salama ukituombea.
Unakumbukwa sana na mke wako Tertula Lyinna, watoto wako Rose, Flora, Juliet, Brenda na Gloria pamoja na wajukuu zako Joan, Michael, Christabell, Malaika, Noela, Cleopatra na Urban. Tunazidi kukuombea upate pumziko la milele.
"Raha ya milele umpe eeh "Bwana na mwanga wa milele umuangazie, upumzike kwa amani.." Amen !
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...