Mkuu wa Wilaya Morogoro, Regina Chonjo (wa pili kushoto) akizungumza jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Doris Mollel, Doris W. Mollel (wa pili kulia), baada ya kupokea msaada ya vitanda vitatu vya kujifungulia wakinamama pamoja na mashine maalum za kuwasaidia watoto wanaozaliwa kabla ya wakati "Njiti" kupumua, Makabidhiano hayo yalifanyika mwishoni mwa wiki katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro. Wengine pichani ni Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dkt. Simon Tarimo (kulia), Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dkt. Ritha Liamue (kushoto), pamoja na Meneja Masoko wa Benki ya CBA, Solomon Kawishe ambao ndio waliofadhili upatikanaji wa vifaa hiyo.
Mkuu wa Wilaya Morogoro, Regina Chonjo (wa pili kushoto) akikabidhi kwa Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dkt. Simon Tarimo (wa tatu kulia) sehemu ya vifaa tiba (vitanda vitatu vya kujufungulia wakina mama pamoja na mashine maalum za kuwasaidia watoto wanaozaliwa kabla ya wakati "Njiti" kupumua), vilivyotolewa na Taasisi ya Doris Mollel kwa ufadhili wa Benki ya CBA kwa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, mwishoni mwa wiki. Wengine pichani kutoka kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Doris Mollel, Doris W. Mollel, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Morogoro, Dkt. Ritha Liamue, Meneja Masoko wa Benki ya CBA, Solomon Kawishe na kushoto ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Morogoro, Ruth John.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Morogoro, Ruth John, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Doris Mollel, Doris W. Mollel pamoja na Meneja Masoko wa Benki ya CBA, Solomon Kawishe wakipanda mti katika eneo la Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, baada ya kukabidhi sehemu ya vifaa tiba (vitanda vitatu vya kujufungulia wakina mama pamoja na mashine maalum za kuwasaidia watoto wanaozaliwa kabla ya wakati "Njiti" kupumua), vilivyotolewa na Taasisi ya Doris Mollel kwa ufadhili wa Benki ya CBA kwa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, mwishoni mwa wiki.
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Doris Mollel, Doris W. Mollel kwa pamoja na Meneja Masoko wa Benki ya CBA, Solomon Kawishe wakimsikiliza mmoja wa wakinamama waliojifungua watoto kabla ya wakati "Njiti" katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, walipotembelea wadi hiyo kutoa zawadi za Sikukuu ya Pasaka kwa wakinamama hao, baada ya kukabidhi sehemu ya vifaa tiba (vitanda vitatu vya kujufungulia wakina mama pamoja na mashine maalum za kuwasaidia watoto wanaozaliwa kabla ya wakati "Njiti" kupumua), vilivyotolewa na Taasisi ya Doris Mollel kwa ufadhili wa Benki ya CBA kwa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, mwishoni mwa wiki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...