Na Humphrey Shao, 
Globu ya Jamii
 Kundi la Waandishi wa habari kumi na Muigizaji mmoja kutoka nchini Israel lililokuja katika utalii wa maeneo mbalimbali nchini limeondoka leo  mara baada ya kumaliza ziara yao ya siku tano nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari mkurugenzi wa Bodi ya Utalii nchini (TTB) Bi. Devotha Mdachi amesema kundi hilo ambalo lilitembea sehemu mbalimbali nchini limewasili jijini Dar es Salaam leo kutoka Kigoma na linataraji kuondoka nchini leo majira ya saa tisa kurudi nchini kwao kwa ndege maalumu ya kukodi.
“Waandishi hawa wa Habari waliofika kufanya utalii nchini ni moja ya matunda yaliyotokana na Rais John Pombe Magufuli kurudisha diplomasia baina ya Islael na Tanzania mara tu walipofungua ubalozi wao hapa nchini hivyo watalii hawa walipata fursa ya kutembelea hifadhi ya Taifa ya Serengeti, visiwa vya Zanzibar na hifadhi ya Sokwe iliyopo Gombe mkoani Kigoma” amesema Bi. Mdachi.
Kwa upande wake afisa habari wa Shirika la Hifadhi ya Taifa nchini (TANAPA), Bw. Pascal Shelutete amesema kuwa watalii hao wamejionea vivutio vingi sana hapa nchini na kusema kuwa kweli nchi hii inahitaji kuitwa nchi ya Asali na Maziwa kama ilivyo kwao.
Amesema kuwa watalii hao wamefuraishwa na jinsi uoto wa asili ulivyo hifadhiwa hapa nchini na kikubwa zaidi kuona sokwe ambao kisayansi inasemekana kuwa wana mahusiano makubwa na wanadamu kwa asilimia 98%.
Kwa upande wake kiongozi wa kundi hilo la watalii hao, Ronit Hershkovitz, amesema kuwa amefurahishwa sana na vivutio vilivyopo hapa na kwa sasa kundi hilo linakwenda kuwa mabalozi kwa watalii wengine wanaotoka ukanda wa Magharibi hasa nchi za Mashariki ya kati.


 Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Nchini (TTB) Bi. Devotha Mdachiakiaga na kiongozi wa kundi la Waaandishi wa habari na watali kutoka nchini Israel Bi. Ronit Hershkovitz kabla ya kuondaka kurudi nchini kwao


 Kiongozi wa kundi la Waaandishi wa habari na watali kutoka nchini Israel Bi. Ronit Hershkovitz  akizungumza  na vyombo vya habari vya hapa nchini kabla ya kuondaka kurudi nchini kwao
 Afisa Habari Shirika la Hifadhi ya Taifa nchini (TANAPA), Bw. Pascal Shelutete akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam wakati akiagana na kundi hilo la Watalii kutoka nchini Islael
 Afisa Habari Shirika la Hifadhi ya Taifa nchini (TANAPA), Bw. Pascal Shelutete akiagana na Kiongozi wa kundi la Waaandishi wa habari na watali kutoka nchini Israel Bi. Ronit Hershkovitz 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...