Na Veronica Simba – Dodoma.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amekataa kusaini ombi la uhamishaji wa leseni ya uchimbaji wa kati wa madini ya Shaba Namba ML 571/2017 kutoka kwa mtanzania David Stanley Kayongoya kwenda Kampuni ya Mechanized Minerals Supreme Mining Company Limited inayomilikiwa na raia kutoka China.

Profesa Muhongo alikataa kusaini leseni hiyo yenye ukubwa wa kilomita za mraba 0.43 katika eneo la Fufu wilayani Chwamwino mkoani Dodoma, baada ya kubaini kuwa mtanzania anayetaka kuhamishia leseni hiyo kwa Raia wa China, hatanufaika kwa kiwango kinachoridhisha.

Akizungumza na wawekezaji mbalimbali wa sekta husika, waliofika Makao Makuu ya Wizara mjini Dodoma, kwa ajili ya kusainiwa leseni zao za uwekezaji, jana (Mei 15), Profesa Muhongo alisisitiza kuwa ni lazima wawekezaji katika sekta husika wazingatie suala la maslahi ya wananchi na Taifa kwa ujumla, wakati wanapotekeleza kazi zao za uwekezaji.

Waziri Muhongo alimwagiza mwekezaji huyo raia wa China kujadiliana kwa mara nyingine na mtanzania mwenye eneo husika (David), ili kuhakikisha ananufaika ipasavyo na uwekezaji huo.

“Ili niweze kusaini leseni hii, rudini mezani, mzungumze na kukubaliana ili David aweze kunufaika. Hatuwezi kukubali kuona watanzania wakidhulumiwa namna hii,” alisisitiza Waziri.
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati), akizungumza na wawekezaji mbalimbali katika sekta ya madini, waliowasilisha maombi ya kupatiwa leseni kwa ajili ya kuwekeza katika sekta husika.
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, akisaini leseni mbalimbali za wawekezaji katika sekta ya madini.

 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akikabidhi leseni ya uchimbaji wa kati wa madini ya ‘Marble’ iliyohamishwa kutoka kwa Salim Mohamed Salum (wa pili kutoka kushoto) kwenda kwa wawekezaji wa kampuni ya S & T Marble and Mining Limited (kulia). Wa kwanza kushoto ni Kamishna wa Madini Tanzania, Mhandisi Benjamin Mchwampaka.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...