Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.


MASHINDANO ya Sprite BBall Kings yameendelea tena jana kwa michezo minne kupigwa katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Airwing.



Ikiwa ni hatua ya pili ya mashindano hayo baada ya wiki iliyopita kupatikana kwa timu 18 zilizoingia baada ya kupigwa michezo takribani 26.

Mchezo wa kwanza uliwakutanisha timu za Dream Chaser na Land Force na timu ya Dream Chaser kuibuka na ushindi wa vikapu 92 dhidi ya 72 za Land Force.

Mechi ya pili iliwakutanisha Kurasini Heat ambaye alitoka na ushindi mnono wa vikapu 124 dhidi ya Bongo Hits aliyepata vikapu 14, The Fighters wakaumana na Chanika Legends na kufanikiwa kushinda kwa vikapu 93 dhidi ya vikapu 16.

Mechi ya mwisho iliwakutanisha TMT na God With Us na kuhitimisha mechi ya nne kwa TMT kuibuka na ushindi wa vikapu 72 dhidi ya 23 huku kukisubiriwa mechi zingine zitakazopigwa wiki ijayo kuwapata washindi wa jumla watakaoingia hatua ya tatu ya mashindano hayo.

Mratibu wa Mashindano hayo ya Sprite BBall Kings Basilisa Biseko amesema kuwa baada ya kumalizika kwa mechi za wiki ijayo timu zilizopata alama nyingi ndiyo zitafanikiwa kuingia hatua inayofuata.

"Timu zilizopata alama nyingi katika michezo ya leo na katika michezo ya wiki ijayo ndiyo watakaofanikiwa kuingia hatua inayofuata ya michuano ya Sprite BBall Kings,"amesema Basilisa.

Michuano hiyo inayodhaminiwa na Sprite kwa kushirikiana na East Africa Tv na Redio inaendelea tena wiki ijayo katika viwanja vya Chuo cha Bandari na mshindi kamili ataondoka na kitita cha shiling milion 15

Timu ya Land Force wakiumana na Dream Chaser katika mechi ya hatua ya pili ya mashindano ya Sprite Bball Kings jana katika Viwanja vya Airwing.
Timu ya Mpira wa Kikapu Dream Chaser.
Mchezaji wa Dream Chaser akifunga kwa mtindo wa kudanki katika mchezo wa hatua ya pili ya mashindano ya Sprite BBall Kings.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...