Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi amemkutana na Mwakilishi mkazi WA Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Watoto duniani-UNICEF bibi Maniza Zaman ofisini kwake mjini Dodoma.
Katika kikao hicho viongozi hao mbali na kufahamiana pia wamejadili namna ya kuboresha mahusiano baina ya Wizara na UNICEF .
Katika maongezi hayo Bi. Zaman aliishukuru Wizara na taasisi zake kwa ushirikiano inayowapa UNICEF katika programu mbalimbali inazoshirikiana na Wizara.
UNICEF inatekeleza kwa kushirikiana na Wizara katika maeneo ya usajili wa watoto chini ya miaka mitano na kuwapa vyeti vya kuzaliwa, huduma ya msaada wa kisheria na mkakati wa haki mtoto.
Prof. Kabudi akiwa na bibi Zaman balsa ya kumaliza mazungumzo ya yaliyofanyika ofisini kwake mjini Dodoma
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...