Baadhi ya Wakandarasi nchini bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo upitaji wa magari makubwa bila ya kuwa na vipimo maalum, hali hiyo imekuwa ikiharibu miundombinu ya barabara,huku wakibainishwa kuwa wamekuwa wakitumia gharama kubwa ya kufanya marekebisho mbalimbali kabla ya kukabidhi barabara hizo kwa Serikali.

Hayo yameelezwa leo na mmoja wakandarasi kutoka Kampuni ya Caberisa Co.Ltd Bernad Mgohamwende ambae anajenga barabara kwa kiwango cha changalawe yenye urefu wa kilomita 36, eneo la barabara ya mbauda ,Osunyai iko katika kiwango cha changarawe,barabara hiyo ipo katika hatua za mwisho kukabidhidhiwa katika wilaya ya Arusha,Mkoa wa Arusha.

Mkanadarasi huyo amesema kuwa katika utekelezaji wa kujenga barabara hizo ,Serikali itaweka utaratibu wa kupima magari hayo ili kusaidia kutunza barabara hizo na wao za kutotumia gharama kubwa kuzirekebisha .

Bila Serikali kuweka vipimo maalumu katika barabara zetu, italazimika kutoa pesa mara kwa mara kuwalipa wakandarasi kwa ajili ya kufanya marekebisho,jambo ambalo itazidi kuitia hasara Serikali na kuwa na matumizi mabaya ya pesa hizo.


Picha ikimuonesha Mkandarasi kutoka Kampuni ya Caberisa Co.Ltd Bernad Mgohamwende, ambaye anajenga barabara kwa kiwango cha changarawe yenye urefu  wa kilomita 36, eneo la barabara ya mbauda ,Osunyai Mkoani Arusha iko katika hatua za mwisho kukabidhi (Picha na Pamela Mollel).


HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...