Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka akizungumza na Waandishi wa Habari wakati akitoa taarifa ya mwenendo wa mchakato wa uchaguzi wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi(UVCCM) na kusema kuwa yoyote atakaye jihusisha na vitendo vya Rushwa asitegemee nafasi ndani ya jumuiya hiyo au chama
Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Shaka Hamdu Shaka, akisisitiza jambo kwa Waandishi wa habari juu ya mwenendo wa Jumuiya hiyo nchini na mafanikio waliyoyapata ndani ya miaka mitatu
Waandishi wa Habari walioshiriki mkutano huo wakifuatilia hotuba ya Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Shakha Hamdu Shakha.
Ndugu Waandishi wa habari;
Kwa mara nyingine tena
tunawakaribisha kwa mikono miwili katika mkutano huu muhimu. Karibuni
sana huku nikiwaomba mjione mko huru na mko nyumbani .
Dhana ya Demokrasia ni jambo
muhimu linalohitaji kuheshimiwa na kuenziwa ndani ya Chama na Jumuiya
zake. Kiongozi wa UVCCM mahali popote pale huchaguliwa kwa kufanyika
uchaguzi huru na wa haki unaozingatia Kanuni na Taratibu za Uchaguzi
kama zilivyoagizwa na vikao husika bila ya kukiuka, kupuuzwa au
kuvunjwa.
Nia ya UVCCM ni kujenga na
kudumisha haiba njema ya kuendelea kuheshimu misingi ya demorasia ya
kweli , yenye kuchunga adabu na kufuata nidhamu, miiko na maadili kwa
kila mwanachama anayetaka kutumia haki ya kuchagua au kuchaguliwa.
April Mwaka 2017 Chama Cha
Mapinduzi kilianza mchakato wa Uchaguzi ndani ya Chama na Jumuiya zake.
Kufuatia mabadiliko ya Kanuni ya UVCCM yaliyofanyika mwezi Machi, 2017
tulianza Uchaguzi katika ngazi za Matawi ambapo hadi leo jumla ya Matawi
23,529 sawa na Asilimia 99.4% kati ya Matawi 23,670 sawa na Asilimia
0.59% yamekamilisha uchaguzi.
Ngazi za Kata 3,913 sawa na
Asilimia 96.59% kati ya Kata 4,051 sawa na asilimia 3.4% zimekamilisha
uchaguzi .Kwa upande wa majimbo ya Zanzibar majimbo 54 sawa na Asilimia
100%, wamekamilisha uchaguzi.
Ngazi ya Wilaya na Mkoa mchakato
wa uchujaji wa majina kwa Vijana waliomba nafasi mbali mbali ndani ya
Jumuiya yetu , umeanza na unaendelea vizuri huku jumla ya Vijana 7,606
wamejitokeza kuchuka fomu za kugombea nafasi mbali mbali katka Jumuiya
yetu, hali inayoonyesha kumekupo kwa mabadiliko na msisimko wa kisiasa
ukilinganisha na chaguzi zilizopita.
Kwa upande wa ngazi ya Taifa Vijana 350 wamejitokeza kuomba nafasi za uongozi ndani ya UVCCM kama ifuatavyo:-
(i) | Nafasi ya Mwenyekiti | 113 | Walioomba |
(ii) | Nafasi ya Makamu Mwenyekiti Taifa | 24 | Walioomba |
(iii) | Nafasi 5 za Wajumbe wa H/Kuu | 103 | Walioomba |
(iv) | Nafasi 5 za Wajumbe wa B/Kuu Taifa | 81 | Walioomba |
(v) | Nafasi 1 Wawakilishi UWT | 14 | Walioomba |
(vi) | Nafasi 1 Wawakilishi Wazazi | 15 | Walioomba |
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...