Mganga Mkuu mkoani Mwanza Dkt.Leonard Subby. |
Madaktari pamoja na Waganga nchini wametakiwa kutumia weledi wa
taaluma yao katika kuhudumia wagonjwa hususani wafanyakazi wanaoumia kazini kwa
kuhakikisha wanapata huduma kwa wakati.
Mganga Mkuu mkoani Mwanza Dkt.Leonard Subby ameyasema hayo leo wakati
akifunga mafunzo ya siku tano kwa madaktari na waganga kutoka mikoa ya Kanda ya
Ziwa yaliyoandaliwa na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi nchini WCF na kufanyika katika ukumbi wa BOT Jijini Mwanza.
Amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo Madaktari pamoja na Waganga
ili kutambua namna bora ya kufanya tathimini kwa mfanyakazi aliyeumia akiwa
kazini.
Dkt.Abisalam Omary ambaye ni Mkurugenzi wa huduma za tiba na tathimini
WCF, amesema mfuko huo unawajengea uwezo madaktari hao ili kufanya tathmini
sahihi kwa wagonjwa wanaoumia kazini ama wasaidizi wao.
Rehema Kabongo ni Meneja wa Mafao ya Fidia Mfuko wa Fidia Kwa wafanyakazi (WCF) anasema kuwa "Tangu mpango huo ulipoanza mwaka 2015 kila uchwao maajiri wamekuwa wakifumbuka macho na kuona haja ya kujiunga na mfuko wa fidia kwa wafanyakazi kiasi kwamba wengi kwa makundi wameanza kujiunga na mfuko"
"Bado tunapata changamoto katika kutoa elimu kwa sababu mfuko huu bado ni mpya lakini tumejipanga kuhakikisha tunawafikia mmoja mmoja au kwa makundi ili kufikia malengo tuliyojiwekea yenye tija kwa matabibu wetu"
“Tunataka hawa madaktari wawe na ujuzi wa kutosha utakaowawezesha kufanikisha azma yetu, na tumeamua kuwa mafunzo ya aina hii yatakuwa endelevu ikiwa ni pamoja na kuwapatia muongozo utakaowasaidia kutekeleza majukumu yao ya kufanya tathmini,” alisema.
Mbali na madaktari na watumishi walio katika sekta ya afya wengi wa wafanyakazi waliopatwa na matatizo hayo kazini wanatoka sekta mbali mbali kama migodi, viwanda na usafirishaji.
Mfuko huo umeingia mkataba na watoa huduma za afya kwenye hospitali na vituo vya afya zaidi ya 6,000 nchi nzima ambapo zitahudumia wafanyakazi hao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...