Na.Vero Ignatus ,Mlandizi

Mkuu wa wilaya ya Kibaha Assumtha mshana amewaasa wanawake kutokudharau kazi hata kama ni ndogo kwani kwenye hiyo ndogo ndipo nyingine kubwa itafuata.

Ameyasema hayo Katika Kanisa la RGC lililopo Mlandizi ambapo alikuwa mgeni rasmi katika Kongamano la wanawake lililoambatana na Changizo kwa ajili ya kununua eneo la kiwanja cha kujenga kanisa

Mkuu huyo wa wilaya ambaye pia ni mchungaji alipata nafasi ya kuhubiri katika kongamano hilo, ambapo amewataka wanawake kujiamini na kuaajibika kwani hata neno la Mungu linasema asiyefanya kazi na asili.

"Nyumba ambayo mwanamke ni legelege nyumba hiyo haitaendelea kamwe,wanawake changamkeni wajibikeni nyie ndiyo nguzo ya familia hutamchosha mume wako" alisema

Kwa upande wake Mchungaji Kiongozi Kambi ya Waebrania Mlandizi Mercy Adam Mwakimomyile amesema kuwa Kongamano hilo limebeba kaulibiu isemayo Nguvu ndani ya Mwanamke(Power in Woman)ambapo imewafanya wanawake wajisikie wanaweza

"Kutokana na uwezo uliopo ndani ya mwanamke basi leo tumeamua kuwa tunaweza kumjengea Mungu madhabahu kupitia kongamano hili" alisema

Amesema katika kanisa hilo wato watoto zaidi ya elfu moja ambao wanafundishwa maadili kupitia neno la Mungu kuibua vipawa  mbalimbali vilivyopo ndani yao na kuviibua
Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Assumta Mshama .Picha na Vero Ignatus Blog.
Mkuu wa wilaya akiweka saini katika kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika kanisa la GRC kambi ya Waebrania Mlandizi àliyepo kulia kwake ni mchungaji kiongozi wa kanisa hilo la Mlandizi.
Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Mhe.Assumtha Mshama akiwa anaonyeshwa mipaka ya eneo la kiwanja cha Kanisa la GRC Kambi ya Warbrania Mlandizi aliyepo nae ni Mchungaji kiongozi wa Kanisa hilo  Mercy Adam Mwakimomyile.Picha na Vero Igbatus Blog.
Mkuu wa wilaya ya Kibaha Mhe.Assumta Mshama akiwa anaongoza maombi mara baada kuona eneo ambalo linatarajiwa kujengwa kanisa .Picha na Vero Ignatus Blog.Kuna Mama Mtume Deo Rwetaka 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...