SHULE mbili za manispaa ya Kinondoni shule ya Kigogo na Mkwawa zaadhimisha siku ya unawaji mikono ambayo hufanyika kila mwaka Oktoba 13 ikiwa na kaulimbiu ya mikono safi kwa manufaa ya sasa na ya baadae.

 Akizungumza wakati wa maadhimisho hayo Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta amesema kuwa kila mtoto anatakiwa kunawa mikono kabla na baada ya kula pamoja na watokapo masalani ili kuepukana na maradhi ya kipindupindi na maradhi yaletwayo kwa kula uchafu.

Amesema kuwa siku hii ni muhimu hasa kwa watoto wanaokurupuka kumegeana vyakula au vitafunwa wawapo shuleni bila ya kunawa mikono yao na bila ya kujua ni nini madhara ya kula bila kunawa.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta akizungumza wakati wa kuadhimisha siku ya kunawa mikono iliyofanyika katika shule ya Msingi Mabibo na shule ya Msingi Mkwawa jijini Dar es Salaam leo.
Pia amewaasa wanafunzi wa shule za msingi Kigogo pamoja na Mkwawa kunawa mikono mikono kila wanapotaka kula na baada ya kula pia marabaada ya kutoka maeneo ambayo wanashika uchafu.
 Wanafunzi wa shule ya Msingi Kigogo na shule ya msingi Mkwawa wakiwa katika siku ya kunawa mikono iliyoadhimishwa shuleni hapo kwaajili kuelewa manufaa ya kunawa mikono kabla ya kula, baada baada ya   kula,  na baada ya kutoka msalani kwaajili ya kujikinga na maradhi yanayoletwa na kuto kunawa mikono.
 Mwanafunz wa chuo Kikuu cha Muhimbili Kerobe  TEHSA akiwafundisha watoto jinsi ya kunawa mikono kwa kutumia kibuyu chirizi ambacho ni rahisi zaidi kuliko kuchota maji kwa kutumia kikombe ambayo ni kwaajili ya kunawa mikono kabla na baada ya kula na wakati watokapo msalani hii ikiwa ni siku ya unawaji Mikono iliyoambatana na kauli mbiu ya Mikono safi kwa manufaa ya sasa na yabaadae.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...