Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi
Kigwangalla akiwaongoza Maafisa wa Wanyamapori 87 wa Mamlaka ya Usimamizi wa
Wanyamapori Tanzania– TAWA, Shirika la Hifadhi za Taifa – TANAPA na Mamlaka ya
Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro kupiga gwaride la ukakamavu muda mfupi baada ya
kuwatunuku vyeti vya kuhitimu mafunzo ya Jeshi Usu jana katika kituo cha Mlele
mkoani Katavi.
Na Hamza Temba- Mlele, Katavi
...........................................................................
WAZIRI wa Maliasili na
Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla amewaagiza wahifadhi wote nchini kushirikiana na
wadau wengine hasa mamlaka za Mikoa na Wilaya katika maeneo yenye uvamizi wa
mifugo na migogoro ya mipaka ya hifadhi ili kutatua changamoto hizo kwa namna
shirikishi ikiwa ni pamoja na kuimarisha utoaji wa elimu kwa wananchi
wanaozunguka maeneo hayo.
Ametoa agizo hilo jana
Disemba, 16, 2017 katika Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi wakati akifunga mafunzo
ya 15 ya mabadiliko ya kuelekea mfumo wa Jeshi Usu kwa Maafisa wa Wanyamapori
87 wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania– TAWA, Shirika la Hifadhi za
Taifa – TANAPA na Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro.
“Kazi ya ulinzi wa
rasilimali zetu za asili ni yetu na tutaiendeleza, Falsafa yetu ni
kuwashirikisha wadau wote, kama kuna taasisi za kiraia kwenye eneo lako la
kazi, taasisi za kijamii, mamlaka za mikoa na wilaya, wananchi, halmashauri
husika mshirikiane nao ili kupunguza madhara ya operesheni zetu, na zoezi hili
la uhifadhi liwe endelevu,” alisema Dk. Kigwangalla.
Aidha, alitoa wito kwa
wananchi wote kuendelea kuheshimu Sheria za nchi na kuacha kufanya shughuli za
kibinadamu kwenye maeneo ya hifadhi ikiwemo kuingiza mifugo, kuanzisha kilimo,
makazi na ukataji wa miti kwa ajili ya kuchoma mkaa na matumizi mengineyo.
Awali akizungumzia
mafunzo hayo alisema, lengo ni kubadilisha utendaji katika sekta ya uhifadhi
kutoka ule wa kiraia kwenda wa jeshi usu ambao utaongeza nidhamu, uwajibikaji,
uadilifu na maadili kwa watumishi wote wa sekta hiyo ili waweze kusimamia
ipasavyo uhifadhi endelevu wa maliasili za taifa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...