NA K-VIS BLOG/Khalfan Said, Mbeya
VIWANGO vya madhara ya kuumia vinahusika sana katika kufikia matokeo ya tathmini anayofanyiwa mfanyakazi aliyeumia mahala pa kazi, Daktari bingwa mbobezi wa mifupa na viungo nchini, Dkt. Robert Mhina, (pichani juu), amesema.
Dkt. Mhina ameyasema hayo wakati akiwasilisha mada juu ya misingi inayopaswa kuzingatiwa na daktari au mtoa huduma ya afya wakati akimfanyia tathmini mfanyakazi aliyeumia mahala pa kazi, kwenye mafunzo ya siku tano yaliyoandaliwa na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), ili kuwajengea uwezo madaktari na watoa huduma za afya kutoka mikoa ya nyanda za juu Kusini yanayoendelea kwenye ukumbi wa Benjamin Mkapa jijini Mbeya.
Akifafanua Dkt. Mhina alisema, Viwango vya fidia vitatofautiana kulingana na viwango vya madhara aliyopata mtu kulingana na kazi anayofanya. “Mfano dereva aliyevunjika mguu ambao anautumia kukanyaga klachi na gia katika kazi yake, fidia yake haiwezi kulingana na mhudumu wa ofisi ambaye naye amevunjika mguu” Alisema na kufafanua kuwa.
“Dereva hawezi tena kuendelea na kazi yake ya udereva kwa vile hana mguu tena ambao aliutegemea kufanya kazi, lakini mhudumu anaweza kutumia gongo na akatembea, ingawa muda wa kufika mahala fulani katika ofisi utakuwa tofauti, lakini anaweza kuhamisha mafaili kutoka sehemu moja kwenda nyingine na kwa maana hiyo bado ataendelea kufanya kazi hiyo tofauti na dereva.” Alisema
Kwa msingi huo, Dkt. Mhina ambaye pia ni mshauri wa masuala ya tiba alisema “Wananchi na wafanyakazi wanapaswa kujua kuwa mafao yatatolewa kutegemea na athari au kazi mtu anayofanya na hayawezi kufanana katika kupiga hesabu za kutoa mafao, kwani kuna vitu vya ziada vinapaswa kuzingatiwa pia.
 Dkt. Hussein Mwanga, akiwasilisha mada juu ya tathmini ya maradhi ya ngozi na kansa mahala pa kazi.
 Afisa Mwandamizi anayeshughulikia madai ya fidia (Claims), Bw.Lembo, akizungumza
 Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusoianio WCF, Bi. Laura Kunenge, akizungumza.


Baadhi ya washiriki

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...