Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
BRITISH Council kupitia mradi wa Connecting Classrooms umetoa mafunzo ya uongozi kwa walimu wakuu wa shule za msingi na sekondari 100 kutoka Wilaya zote za Mkoa wa Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa British Council lengo la mafunzo hayo ni kuendelea kuwajengea uwezo walimu hao katika masuala ya uongozi, ufundishaji bora  na mbinu bora za kufundisha wanafunzi ili wafaulu kwenye masomo yao.

Akizungumza  katika Shule ya Sekondari Mzimuni ambako ndiko mafunzo hayo yalikuwa yakitolewa kwa siku tatu, Meneja Mradi wa Connecting Classrooms Ephraim Kapungu amesema kupitia mradi huo wamefanikiwa kufikia walimu wengi 100 kwenye mkoa wa Dar es Salaam.

"Tumetoa mafunzo haya kwa walimu wakuu shule za msingi na sekondari kwa walimu hao.Lengo letu ni kuwajengea uwezo katika masuala ya uongozi hasa kwa kuzingatia mradi huo unatambua umuhimu wa walimu wakuu kuwa na mafunzo ya aina hiyo.

"Tunaamini kupitia mafunzo haya ya uongozi walimu wakuu watakuwa na fursa ya kuweza kuongoza shule zao kwa umakini wa hali ya juu na kufanya shule hizo kuwa watulivu na kujikita kwenye kutoa elimu iliyo bora,"amesema Kapungu.
 Afisa Mkuu wa Idara ya Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika kutoka Manispaa ya Kinondoni,Saleh Hijja Mohamed (aliyesimama) akizungumza kabla ya kumalizika kwa semina ya siku tatu ya mafunzo ya uongozi kwa walimu wa shule za msingi na sekondari wa Jiji la Dar es Salaam leo. Semina hiyo imefanyika katika Kituo cha Walimu cha Mzimuni kilichopo Magomeni Mapipa. Kulia wanaoshuhudia ni Afisa Mkuu wa Miradi wa Shirika lisilo la Kiserikali la British Council,Atiya Sumar na Meneja Miradi wa Shirika hilo,Ephraim Kapungu. Picha na Elisa Shunda
 Afisa Mkuu wa Miradi wa Shirika lisilo la Kiserikali la British Council, Atiya Sumar akizungumza katika ufungaji wa semina hiyo.
 Meneja Miradi wa Shirika Lisilo la Kiserikali la British Council, Ephraim Kapungu (katikati) akielezea utendaji kazi wa shirika hilo katika uwezeshaji wa masuala mbalimbali yahusuyo elimu jinsi shirika hilo linavyofanya kazi zake kwa kushirikiana na serikali kupitia wizara ya elimu.
 Mmoja kati ya wakufunzi wa semina hiyo Ndg.Edwin Shunda akiwa katika majukumu yake ya ufundishaji na uwezeshaji wa uongozi kwa walimu wakuu wa shule za msingi na sekondari wa Jiji la Dar es Salaam.
Mgeni rasmi, Afisa Mkuu wa Idara ya Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika kutoka Manispaa ya Kinondoni,Saleh Hijja Mohamed (katikati) akiwa na viongozi wa shirika la British pamoja na walimu wakuu wa shule za msingi na sekondari katika picha ya pamoja baada ya kumalizika kwa semina ya siku tatu ya mafunzo ya uongozi kwa walimu hao wa Jiji la Dar es Salaam.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...