WAZIRI wa Maji na Umwagiliaji,Aisack Kamwelwe ameiagiza Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (Takukuru) kuukagua mradi wa maji wa Buchosa uliopo Wilaya ya Sengerema Mkoani Mwanza kwani anazotaarifa kuna vifaa vimenunuliwa havina ubora kabisa.

Maagizo hayo aliyatoa jana Mjini hapa wakati akizindua ripoti na utendaji wa Mamlaka za Maji za Miji na Mikoa na miradi ya kitaifa.


Uzinduzi huo uliandaliwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) ambapo Mamlaka ya Maji ya Moshi ilichaguliwa kuwa ya kwanza kwa utoaji bora wa huduma za maji. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Isack Kamwelwe (kulia) akimkabidhi tuzo ya ushindi wa Mamlaka inayotoa huduma bora za Maji Tanzania, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Mjini Moshi (MUWSA) ,Prof. Faustine Bee. Kushoto ni Mkurugenzi Mkurugenzi Mkuu wa MUWSA, Joyce Msiru. Makabidhiano hayo yalifanyika mjini Dodoma juzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...