Baraza hilo lenye wajumbe 12 likiwa na mwenyekiti,makamu mwenyekiti,katibu na mweka hazina na wajumbe sita mmoja kutoka kila halmashauri na watoto wawili wanaowakilisha watoto wenye ulemavu. 

Akizungumza wakati wa kuzindua baraza hilo, mjini Shinyanga, Dk. Ndugulile aliupongeza uongozi wa mkoa wa Shinyanga na kuutaka kuendelea kulea baraza hilo na mikoa mingine kuanzisha mabaraza ya watoto. 

“Wizara inaunga mkono kuanzishwa kwa baraza hili na tumetoa kompyuta moja itakayotumika kwa kazi za baraza,tunapenda kuona haki za watoto zinalindwa na ni wajibu wa kila mmoja kuwalinda watoto ili kuhakikisha haki zao hazivunjwi”,alieleza. 

“Naomba wajumbe wa baraza hili muwe mabalozi wa watoto wengine,heshimuni wazazi na walezi,nendeni shule na mjijenge katika maadili na tabia njema,msikae kimya, mpoona haki zenu zinavunjwa toeni taarifa,serikali ipo tuna sheria za kuwalinda”,aliongeza Dk. Ndugulile. 
Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dk. Faustine Ndugulile leo Jumatatu Februari 19,2018 amezindua Baraza la Watoto Mkoa wa Shinyanga na kukabidhi rasmi ofisi na kompyuta kwa ajili ya baraza hilo. 
Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dk. Faustine Ndugulile akizungumza wakati wa kuzindua Baraza la Watoto mkoa wa Shinyanga leo Jumatatu Februari 19,2018 katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga.Kushoto ni ni Kamishina wa Ustawi wa Jamii Dk. Naftali Ngo'ndi ,kulia ni Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga Albert Msovela - Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog 
Wawakilishi wa watoto wanaounda baraza la watoto mkoa wa Shinyanga wakimsilikiza Dk. Faustine Ndugulile. 
Dk. Faustine Ndugulile akizungumza wakati wa uzinduzi wa baraza la watoto mkoa wa Shinyanga.Wa kwanza kulia aliyeinama ni Mganga Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Rashid Mfaume. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...