Ubalozi wa Kuwait nchini Tanzania uliandaa hafla ya kuadhimisha miaka 57 ya Uhuru wa Kuwait, miaka 27 ya Ukombozi na miaka 12 tangu Mfalme wa Kuwait Mheshimiwa Sheikh Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-Sabah apokee uongozi wa nchi hiyo. 
Hafla hiyo ilihudhuriwa na wageni waalikwa mbalimbali wakiongozwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dr. Suzan Kolimba, Waziri mkuu mstaafu Dr.Salim Ahmed Salim, Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Zubeir Ali Maulid, Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir bin Ally, Naibu Waziri wa Ndani Mhandisi, Hamad Masauni pamoja na viongozi wa juu wa serikali, mabalozi wa nchi za kigeni na mashirika ya kimataifa na wataalamu wa fani mbalimbali na vyombo vya habari

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...