Mwanasheria na Wakili wa Masuala ya haki za Watoto, Gebra Kambole akizungumza na wajumbe wa Mkutano wa Wadau wanaopinga ndoa za utotoni katika mkutano Maalum ulioandaliwa na Tasisi ya Msichana Initiative Dar es Salaam, katika Mkutano huo wadau wameweza kujadili na kupitia Rufaa iliyowekwa na Mwanasheria Mkuu juu ya kupinga hukumu iliyotolewa na Mahakama kuu kuwa Mtoto wa Miaka 15 awezi kuolewa.
Afisa Mawasiliano wa , Eileen Mwalongo, akizungumza jambo kuhusiana kupinga ndoa za utotoni wakati wa kikao cha Wadau kujadili Rufaa ya Mwanasheria Mkuu dhidi ya Hukumu ya kesi ya kupinga ndoa kuanzia miaka 15.
Sehemu ya Wadau walioshiriki katika kikao cha Wadau kupinga Rufaa ya Mwanasheria Mkuu kupinga hukumu ya Mahakama kuu juu ya ndoa kuanzia miaka 15.
Sehemu ya Wadau walioshiriki katika kikao cha Wadau kupinga Rufaa ya Mwanasheria Mkuu kupinga hukumu ya Mahakama kuu juu ya ndoa kuanzia miaka 15 wakimsikiliza Mwanasheria Gebra Kambole.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...