OPERESHENI ya nchi nzima kuwabaini waajiri ambao hawatekelezi sheria ya ajira na mahusiano kazini na wale ambao bado hawajajisajili na Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, (WCF), inayoongozwa na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia Kazi, Ajira na Vijana, Mhe. Antony Mavunde, imeingia Mkoani Morogoro leo Machi 9, 2018, ambapo waajiri wamechukuliwa hatua mbalimbali za kisheria ikiwa ni pamoja na kutozwa faini. 

Operesheni hiyo iliyoanzia jijini Mwanza Februari 26, 2018 inafuatia agizo alilolitoa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama, jijini Mbeya mwishoni mwa mwaka jana ambapo aliagiza waajiri ambao bado hawajatekeleza Sheria ya Fidia Kwa Wafanyakazi, Sura 263 marejeo ya mwaka 2015, ambayo inamtaka kila mwajiri kutoka sekta ya umma na binafsi Tanzania bara awe amejisajili na kuwasilisha michango kwenye Mfuko huo, wafikishwe mahakamani. 

Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, (WCF), Bi. Rehema Kabongo, ambaye anafuatana na Mhe. Mavunde kwenye ziara hiyo ya kushtukiza, kuna jumla ya waajiri 536, na kati ya hao ni waajiri 294 tu ndio waliojisajili na Mfuko huku wengine 242 bado hawajatekeleza takwa la kisheria la kujisajili na Mfuko. 

“Naagiza waajiri hawa ambao bado hawajajisajili na Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, wanaofikia 242 wafikishwe mahakamani mara moja ili wakajibu mashtaka kwanini hawajatimiza wajibu wao wa kisheria.” Aliagiza Mhe. Mavunde. 
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Antony Mavunde, akizungumza na wafanyakazi wa kiwanda cha Tumbaku Alliance One Mkoani Morogopro leo Machi 9, 2018. Mhe. Mavunde ameagiza waajiri 242 Mkoani Morogoro ambao hawajajisajili na Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, (WCF) kufikishwa mahakamani mara moja.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Antony Mavunde, (kushoto), akizungumza na Mwenyekiti wa chama cha wafanyakazi, kiwanda cha Tumbaku Mkoani Morogoro, Ujaicy Kayera leo Machi 9, 2018 wakati wa ziara yake ya kushtukiza aliyoifanya Mkoani humo ili kubaini waajiri ambao bado hawajajisajili na Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, (WCF), na wale ambao hawatekelezi Sheria ya Kazi na Mabhusiano Kazini. Mhe. Mavunde ameagiza waajiri 242 ambao hawajajisajili na Mfuko kufikishwa mahakamani mara moja.
Naibu Waziri Antoni Mavundeakizungumza na Meneja wa Kampuni ya Hood, Faisal Hood. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, (WCF), Bi.Rehema Kabongo
Naibu Waziri akiwasli kwenye Kiwanda cha kusindika Tumbaku cha Alliance kilichopo Kingolwira, ambapo alizungumza na wafanyakazi na kubaini makosa ya kiutendaji kwa muajili.
Naibu Waziri akiwasli kwenye Kiwanda cha kusindika Tumbaku cha Alliance kilichopo Kingolwira, ambapo alizungumza na wafanyakazi na kubaini makosa ya kiutendaji kwa muajili.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...