Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

CHAMA Cha Mapinduzi(CCM), Mkoa wa Dar es Salaam kimetoa pole kwa familia ambazo zimepoteza ndugu zao kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha huku kikitoa ushauri kwa Serikali kuwaondoa waliojenga kwenye njia za maji kwa lengo la kupunguza maafa.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam Cylivia Katekamba amewaambia leo waandishi wa habari kuwa chama hicho kinatoa pole kwa wote ambao wamefikwa na maafa na kuomba wenye uwezo wa kusaidia walioathrika na mvua hizo kujitokeza kusaidia.

" Mkoa wa Dar es Salaam umekumbwa na mafuriko na kusababisha baadhi ya wananchi kupoteza maisha.CCM mkoa tunatoa pole kwa ndugu, jamaa na marafiki kutokana na kuondokewa na ndugu zetu kutokana na mvua.

"Tunafahamu matatizo ya mafuriko yametokea kwetu na hata maeneo mengine duniani nayo wakati mwingine hukumbwa na mafuriko.Kubwa ni kuendelea kushikamana na kusaidia kwenye kipindi hiki.CCM tunatoa pole,"amesema Katekamba.

Pia ametoa mwito kwa walio maeneo hatarishi ni vema wakaondoka maeneo hayo na kufafanua kutokana kuzibwa kwa mitaro na njia za maji imesababisha hata maeneo ambayo huwa hayapati mafuriko safari hii maji yamejaa.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Mkoa wa Dar es Salaam Cylivia Katekamba(wa kwanza kushoto) akizungumza ma waandishi wa habari leo jijini wakati anatoa pole kwa waliokumbwa na mafuriko na familia ambazo zimepoteza wapendwa wao kwasababu ya mvua zinazonyesha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...