Na Agness Francis, Blogu ya Jamii
RAIS wa Serikali ya Awamu ya Tano Dk. John Mgufuli  kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya uhuru wa habari  Nchini ambayo kitaifa yatafanyika Mkoani Dodoma  Mei 2 hadi 3  mwaka huu ikiwa ndio kilele chake na kauli mbiu inasema  ni wajibu wa Serikali vyombo vya habari haki na utawala wa sheria.

Ambapo  wageni  zaidi ya 300 wanatajiriwa kuhudhuria  hafla hiyo wakiwepo wadau , wanahabari  ,wabunge na taasisi mbalimbali ambapo kimataifa Afrika  inafanyika Nchini Ghana Accra zaidi ya nchi 100  zitawakilisha katika hafla hiyo.

Akizungumza  jjjini Dar es Salaam Mwenyekiti wa Taasisi  ya vyombo vya habari Kusini mwa Jangwa la Sahara Salome Kitomari amesema katika siku hizo watazungumzia umuhimu wa  uhuru wa habari, utawala bora kwa waandishi wa habari na  wanasheria kama Mahakama kuwa na uhuru  wa kusimamia kesi za jinai za kuwa na uwazi kwa wanahabari vilevile na kukumbusha kutekeleza majukumu katika  uandikaji wa habari kuwa sahihi.

Aidha Makamo wa Rais wa Umoja wa Klabu za waandishi wa habari Jane Mihanji amesema wao wamekuwa na jukumu la kuwaweka pamoja waandishi wa  habari  na kuwapa mafunzo na  kuwapatia  vitendea kazi.
Mwenyekiti wa MISA Tanzania Bi. Salome Kitomari akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya maadhimisho ya uhuru wa habari  Nchini ambayo kitaifa yatafanyika Mkoani Dodoma  Mei 2 hadi 3  mwaka huu na kauli mbiu inasema  ni wajibu wa Serikali vyombo vya habari haki na utawala wa sheria.
Makamu wa Rais wa  Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Jane Mahanji akizungumza na waandishi wa habari namna wanavyokwenda begakwabega na waandishi kwa kuto semina ili kutoa habari zenye faida kwa Taifa.
Mkurugenzi wa  Tanzania Media Foundation (TMF) Fausta Musokwa akizungumza na waandishi wa habari wanavyochangia kwa kiasi kikubwa vyombo vya habari kwa kutoa pesa ili vyombo hivyo vijiendeshe.
Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Stella Vuzo akizungumza na waandishi wa habari kuhusuumoja wa Mataifa unavyodhamini mchango mkubwa wa waandishi wa habari wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuelekea siku ya uhuru wa vyombo vya habari hapa nchini.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...