Na Stella Kalinga, Simiyu
Wafanyabiashara wa Mkoa wa Simiyu wamekubali kuunga mkono Serikali katika Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Mkoa wa Simiyu inayotarajiwa kuanza kujengwa mwezi Juni mwaka huu.

Kauli hiyo ilitolewa na Wafanyabiashara hao katika kikao chao na Mkuu wa Mkoa kilichofanyika  jana Mjini Bariadi, ambacho kilifanyika kwa lengo la kuzungumzia fursa za biashara na uwekezaji zilizopo mkoani humo, changamoto zinazowakabili na utatuzi wake.

Awali akifungua kikao hicho, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka amesema Serikali mkoani humo imekusudia kuwa na shule kubwa itakayoweza kuchukua wanafunzi 1000 ambayo itakayopatikana kwa kujenga upya shule ya Sekondari Simiyu (Kidato cha kwanza hadi cha Nne), ambapo aliahidi kuwa ofisi yake itatoa fedha kiasi na akawaomba wafanyabiasha wazawa kuchangia Ujenzi wa shule hiyo kwa ajili ya maendeleo ya Mkoa.

Amesema  pamoja na kujenga upya Shule ya Sekondari Simiyu, katika shule hiyo kutajengwa mabweni kwa ajili ya wanafunzi wa kike ili wanafunzi wote wa kike wasome wakiwa wanafunzi wa bweni(boarding).

 Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara Mkoa wa Simiyu ambaye pia ni Mbunge wa Itilima Mhe. Njalu Silanga akizungumza katika kikao cha Wafanyabiashara wa Mkoa huo na Mkuu wa Mkoa huo katika Kikao kilichofanyika jana Mjini Bariadi.
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akizungumza na Wafanyabiashara wa Mkoa huo katika kikao kilichofanyika Mjini Bariadi.
 Baadhi ya Wafanyabiashara wa Mkoa wa Simiyu, wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(hayupo pichani) katika kikao chao na Mkuu huyo wa Mkoa kilichofanyika jana Mjini Bariadi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...