Balozi wa Tanzania nchi India Mhe.  Baraka Luvanda ametembelea na kuhudhuria  hafla ya wanafunzi wa Kiafrika wanaosoma kozi mbalimbali katika vyuo jimboni Punjab. 
Hafla hii iliofanyika Mei18, 2018 ilijumuisha wanafunzi karibu wote wa Kitanzania wanaosoma Punjab. Ilijumuisha vyuo kama Gian Jyoti institute of management and technology( chuo kilichoandaa event) ambacho ni miongoni mwa vyuo bora vya masomo ya biashara nchini India,  CDac na vyuio vinginevyo.  
Hafla iliandaliwa na mwanafunzi Bakari Chuma wa mwaka wa pili anaesomea course ya MBA  akishirikiana  na uongozi wa chuo Gian Jyoti Institute of Management and Technology.
 Balozi wa Tanzania nchini  India Mhe. Baraka H. Luvanda wakiwa na mwambata wa elimu Bw. Yahaya A Mhata, Mwenyekiti wa Gian Jyoti groups of institutions  Bw. J. S. Bedi na  Dean wa wanafunzi wa kimataifa Gurdeepak Singh na  baadhi ya wanafunzi wa Kitanzania Mariam Sunday na Vivian Omar na wengine kutoka mataifa mbalimbali. 
 Balozi Luvanda akiwa katika kilemba cha asili akikaribishwa na wenyeji
 Balozi Luvanda akiwa ndugu Yahaya A Mhata  pamoja na  Mr j. S. Bedi chairman na Mkurugenzi Dr Aneet (saree ya njano) wakifurahi na wanafunzi
 Balozi akiwa na wanafunzi wa Kitanzania wanaosoma Punjab.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...