Warsha
hiyo iliyoandaliwa na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania tawi la Shinyanga
kwa ufadhili wa benki ya CRDB tawi la Shinyanga imefanyika leo Jumatatu
Mei 14,2018 katika chuo hicho mjini Shinyanga kwa kukutanisha walimu
100.Warsha hiyo ni sehemu ya Mpango Maalumu uliobuniwa na Chuo hicho kwa
ajili ya kujenga uwezo watumishi wa umma hasa walimu juu ya masuala ya
jinsia.
Akifungua
warsha hiyo,Matiro alisema mbinu stahiki za kupambana na ukatili wa
kijinsia zitafanikiwa endapo dhana,aina,matokeo na sababu za ukatili
zitaeleweka kuanzia ngazi ya msingi hususani shuleni ambapo watoto
wanatumia muda mwingi wa maisha yao.“Niwapongeze sana kwa kuanzisha
mpango huu wa kuwafikia walimu,warsha hii ni nyeti sana na huenda kuna
walimu ambao walishawahi kushuhudia ama kutenda vitendo vya kibaguzi kwa
watoto kwa kujua ama kutojua,kwa hali hii vitendo hivyo vina athari
kubwa katika maendeleo ya kitaaluma kwa watoto”,alisema Matiro.
Aidha
alisema ni jukumu la walimu na shule kuweka kanuni na taratibu ambazo
zitatoa ulinzi na kusaidia jamii nzima ya shule kuishi kwa amani na
kuzingatia usawa.“Niwaombe msiishie kwa walimu pekee kutoa elimu
hii,bali wafikieni pia watumishi wote wa umma kwani nao kwa sehemu yao
wana mchango mkubwa katika ujenzi wa jamii inayothamini usawa wa
kijinsia”,aliongeza.
Mheshimiwa
Josephine Matiro akizungumza wakati wa warsha hiyo.Kushoto ni Mratibu
wa Masuala ya Jinsia katika Chuo Kikuu Huria cha Tanzania tawi la
Shinyanga,Getrude Pastory Massawe ambaye pia Afisa Masoko wa chuo
hicho.Kulia ni Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Chuo Kikuu Huria cha
Tanzania,Kituo cha Shinyanga, Paschal Mheluka.
Mkuu
wa wilaya ya Shinyanga Mheshimiwa Josephine Matiro akizungumza katika
warsha hiyo na kueleza kuwa kukosekana kwa usawa baina ya wasichana na
na wavulana shuleni na katika jamii ni chanzo kikuu cha ukatili kitu
kinachofanya ukatili kuwa suala la kijinsia.
Mwakilishi
wa Mkurugenzi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania,Kituo cha Shinyanga,
Paschal Mheluka akizungumza wakati wa warsha hiyo iliyokutanisha walimu
100 kutoka shule za msingi na sekondari zilizopo katika manispaa ya
Shinyanga.
Mratibu
wa Masuala ya Jinsia katika Chuo Kikuu Huria cha Tanzania tawi la
Shinyanga,Getrude Pastory Massawe ambaye pia Afisa Masoko wa chuo hicho
akizungumza wakati wa warsha hiyo ambapo alisema wameamua kuanzisha
mpango wa kutoa elimu ya masuala ya jinsia kwa walimu ili kuhakikisha
walimu hao wanatoa elimu kwa wanafunzi wao kumaliza vitendo vya ukatili
katika jamii.
Washiriki wa warsha hiyo wakiwa ukumbini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...