Na mwandishi wetu
Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir Bin Ally amesema Waislamu na walimwengu kwa ujumla wananafasi kubwa ya kujifunza mawaidha yanayotolewa katika mwezi Mtukufu wa Ramadhani ikiwamo kumcha Mungu na uadilifu.

Mufti alisema hayo kwenye futari iliyoandaliwa na benki ya Standard Chartered katika hoteli ya Serena.

Alisema katika hafla hiyo ambayo pia walikuwemo wageni wastahiki Balozi wa Indonesia nchini Tanzania, Mheshimiwa Prof. Dk. Ratlan Pardede na Balozi wa Heshima wa Siera Leone nchini Tanzania, Hussein Hamadi, kuwa mwezi wa Ramadhani ni chuo ambacho kinafunza mambo mbalimbali.

Alisema mafunzo hayo yanatarajiwa kutumika muda wote katika miezi 11 iliyobaki katika mwaka.

Alisema mambo ambayo yanazungumzwa katika Chuo hicho ni mengi lakini makubwa ni mahusiano katika masuala ya kiroho, kijamii, kiuchumi na kimaadili.

Alisema mafunzo yanayopatikana katika mwezi huo mmoja wa kumcha Mungu wenye siku takribani 29 hadi 30 yanatengeneza uaminifu si kwa Mungu pekee bali na kwa viumbe wake.
 Mgeni rasmi Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir Bin Ally akitoa mawaidha kwa wateja wa benki ya Standard Chartered wakati wa futari iliyoandaliwakwa wateja wa benki hiyo katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered nchini, Sanjay Rughani akizungumza na wateja pamoja na wageni waalikwa wakati wa futari iliyoandaliwa kwa wateja wa benki hiyo katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Balozi wa Indonesia nchini, Prof Dk Ratlan Pardede akizungumza na wateja wa benki ya Standard Chartered wakati wa futari iliyoandaliwa kwa wateja wa benki hiyo katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Balozi wa Heshima wa Siera Leone nchini, Mh. Hussein Hamadi akitoa salamu za mwezi Mtukufu wa Ramadhani kwa wateja wa benki ya Standard Chartered wakati wa futari iliyoandaliwa kwa wateja wa benki hiyo katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered nchini, Sanjay Rughani akibadilishana mawazo na mgeni rasmi Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir Bin Ally (kulia) wakati wa futari iliyoandaliwa kwa wateja wa benki ya Standard Chartered katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Kutoka kulia kwenda kushoto ni Mgeni rasmi Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir Bin Ally, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered nchini, Sanjay Rughani, Balozi wa Indonesia nchini, Prof Dk Ratlan Pardede pamoja na Balozi wa Heshima wa Siera Leone nchini Hussein Hamadi wakiwa meza kuu wakati wa futari iliyoandaliwa kwa wateja wa benki hiyo katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Pichani juu na chini ni baadhi ya wateja na wadau wa benki ya Standard Chartered waliohudhuria futari iliyoandaliwa na benki hiyo katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

 Mgeni rasmi Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir Bin Ally katika picha ya pamoja na meza kuu na baadhi ya viongozi wa Bakwata mara baada ya kumalizika kwa futari iliyoandaliwa kwa wateja wa benki ya Standard Chartered katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...