Na Mwandishi wetu
TAASISI ya Dr Ntuyabaliwe imezindua shindano la Andika Challenge kwa watoto wa shule za msingi manispaa ya Kinondoni wenye lengo la kuibua vipaji vya watoto katika kubuni na kutunga hadithi.

Shindano hilo linatarajiwa katika siku za usoni kufika Tanzania nzima.

Uzinduzi huo umefanywa katika shule ya msingi Kinondoni wilayani Kinondoni.

Akizindua shindano hilo Kaimu Afisa Elimu Manispaa ya Kinondoni, Esther Kaaya alisema shindano hilo ni muhimu kwa nchi hii hasa katika kukuza uwezo wa kusoma na kuandika na kuibua vipaji vya wanafunzi katika kukuza lugha ya Kiswahili na ubunifu.

Alisema kwamba serikali inafurahishwa na jinsi taasisi hiyo inavyofanywa ya kuibua vipaji vya watoto na kukuza lugha ya Kiswahili kwa kuangalia usomaji wa vitabu na shindano la andika challenge.

Alisema anajua kwamba Taasisi hiyo ilianza na maktaba katika shule za msingi na kuhamasisha usomaji wa vitabu na sasa wanakuja na shindano hilo litakalosambaa nchi nzima.

Alisema andika challenge ni muhimu kwa watoto.

“Tunaamini kuwa tunaenda kukuza vipaji vya watoto…katika kutunga hadithi kwa kuongoza watoto katika kuhakikisha kwamba uchaguzi wa mada zinakuwa na maana zikizingatia fani na maudhui, moja ya tanzu au kipera cha simulizi “ alisema.
 Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Kinondoni, Bw Emmanuel Ntenga akizungumza machache na kuitambulisha meza kuu wakati wa hafla ya uzinduzi wa shindano la Andika Challenge kwa watoto wa shule za msingi manispaa ya Kinondoni iliyofanyika mwishoni mwa wiki shuleni hapo jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Mtendaji wa Kata ya Mwananyamala, Mickidadi Ngatumbura, Mgeni rasmi Kaimu Afisa Elimu Manispaa ya Kinondoni, Esther Kaaya, Mkurugenzi wa Taasisi ya Dr Ntuyabaliwe, Bi. Jacqueline Mengi pamoja na Afisa Elimu kata ya Mwananyamala, Joshua Biswalo wakiwa meza kuu.
 Mgeni rasmi Kaimu Afisa Elimu Manispaa ya Kinondoni, Esther Kaaya akizungumza na wanafunzi pamoja na walimu wa shule ya msingi Kinondoni wakati wa hafla ya uzinduzi wa shindano la Andika Challenge kwa watoto wa shule za msingi manispaa ya Kinondoni iliyofanyika mwishoni mwa wiki shuleni hapo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Dr Ntuyabaliwe, Bi. Jacqueline Mengi pamoja na  Mtendaji wa Kata ya Mwananyamala, Mickidadi Ngatumbura (kushoto).
 Mgeni rasmi Kaimu Afisa Elimu Manispaa ya Kinondoni, Esther Kaaya akitoa mkono wa pongezi kwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Dr Ntuyabaliwe, Bi. Jacqueline Mengi wakati wa hafla ya uzinduzi wa shindano la Andika Challenge kwa watoto wa shule za msingi manispaa ya Kinondoni iliyofanyika mwishoni mwa wiki shuleni hapo jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Taasisi ya Dr Ntuyabaliwe, Bi. Jacqueline Mengi akizungumza kuhusu vigezo vya kushiriki na zawadi kwa tano bora kwa wanafunzi wa shule za msingi manispaa ya Kinondoni watakaoshiriki shindano la Andika Challengekatika hafla fupi ya uzinduzi huo iliyofanyika kwenye ukumbi wa maktaba ya shule ya msingi Kinondoni mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Mwanafunzi Brian Jackson wa darasa la saba shule ya msingi Kinondoni akitoa neno loa shukrani kwa Taasisi ya Dr. Ntuyabaliwe kwa kuzindua shindano hilo la andika challenge wakati hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa maktaba shuleni hapo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwanafunzi Blessing Elianoki wa darasa la sita.
 Mgeni rasmi Kaimu Afisa Elimu Manispaa ya Kinondoni, Esther Kaaya pamoja na Mkurugenzi wa Taasisi ya Dr Ntuyabaliwe, Bi. Jacqueline Mengi wakizundua shindano la andika challenge kwa watoto wa shule za msingi manispaa ya Kinondoni katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa maktaba shuleni hapo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Sehemu ya waandishi wa habari na baadhi ya walimu wa shule ya msingi Kinondoni waliohudhuria uzinduzi wa shindano la andika challenge kwa watoto wa shule za msingi manispaa ya Kinondoni katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa maktaba shuleni hapo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Kinondoni waliowakilisha wenzao katika hafla fupi ya uzinduzi wa shindano la andika challenge kwa watoto wa shule za msingi manispaa ya Kinondoni iliyofanyika kwenye ukumbi wa maktaba shuleni hapo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Taasisi ya Dr Ntuyabaliwe, Bi. Jacqueline Mengi katika picha ya pamoja na baadhi ya walimu wa shule ya msingi Kinondoni mara baada ya kumalizika kwa hafla ya uzinduzi wa shindano la andika challenge kwa watoto wa shule za msingi manispaa ya Kinondoni uliofanyika kwenye ukumbi wa maktaba shuleni hapo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Taasisi ya Dr Ntuyabaliwe, Bi. Jacqueline Mengi katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi na baadhi ya walimu wa shule ya msingi Kinondoni mara baada ya kumalizika kwa hafla ya uzinduzi wa shindano la andika challenge kwa watoto wa shule za msingi manispaa ya Kinondoni uliofanyika kwenye ukumbi wa maktaba shuleni hapo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Dr Ntuyabaliwe, Bi. Jacqueline Mengi katika picha ya pamoja na mgeni rasmi Kaimu Afisa Elimu Manispaa ya Kinondoni, Esther Kaaya, Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Kinondoni, Bw Emmanuel Ntenga pamoja na baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo waliowakilisha wenzao katika hafla fupi ya uzinduzi wa shindano la andika challenge kwa watoto wa shule za msingi manispaa ya Kinondoni uliofanyika kwenye ukumbi wa maktaba shuleni hapo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...