JOSEPH MPANGALA,MTWARA

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara DCP Lucas Mkondya amewaonya Madereva wa Magari na Pikipiki Kuacha Kutumia Kilevi na baadaye Kuendesha Hasa katika Sikukuu ijayo ya Idd El Fitri.

Akiongea na waandishi wa habari Ofisini kwake Kamanda Mkondya amewataka watu woote wanaotumia Kilevi kuhakikisha wanatafuta madereva watakao wandesha kwa lengo la kuepuka Ajali.

“Tukikumata umelewa na unaendesha gari Utakaa mahabusu ya Polisi Mpaka Sikukuu itakapokwisha ndio tutakupeleka Mahakamani,Kwa hiyo Tukikukamata siku ya Iddi Utakuja kupelekwa Mahakaman siku ya Jumatatu lakini kama unaona Huwezi Sikumbili haziwez kupita Bila kunywa Pombe ni Bora Utafute Dereva aweze kukuendesha”

Aidha ameongeza kuwa katika siku ya Idi Watu woote wanaopenda kukaa maeneo ya ufukweni wahakikishe wanaondoka na kurudi majumbani Pindi inapofika Mida ya saa 12 Jioni.

“Inapofika Saa12 jioni hatutaruhusu watu kuendelea kuogelea baharini kwa hiyo tunawaomba waende mapema na itakapofika saa12 jioni werejee majumbani”

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...