Wafanyakazi wa TMA wakishiriki katika zoezi la kupanda miti wakiongozwa na Mkurugenzi Mkuu Dkt. Agnes Kijazi.

Na Monica Mutoni

WAKATI huu ambapo tunaadhimisha wiki ya mazingira ni vyema tukakumbuka tulikotoka, wakati wazee wetu wakitumia busara zao kutushauri kutunza mazingira ili yatutunze.

Moja ya msisitizo wao ulikuwa ni pamoja na kutuaminisha kwamba utunzaji wa mazingira ni kupanda miti, lakini umefika wakati na sisi tujiulize kupanda miti ndio utunzaji wenyewe wa mazingira? 

Kwa mujibu wa wataalamu wa mazingira, ushauri wa wazee juu ya kupanda miti ni sahihi kabisa, nadharia ambayo pia inaungwa mkono na wataalamu wa hali ya hewa kote duniani ambao wanaamini maeneo yenye misitu mizito, ndiko kunapokuwa na mvua nyingi zaidi. 

Wataalam hao wanatolea mfano wa misitu mikubwa duniani ikiwemo misitu ya Congo ambapo wanasema pamoja na kupata mvua nyingi maeneo hayo  yanakuwa na hewa safi kulinganisha na maeneo ambayo hayana misitu kwani miti ina tabia ya kuondoa hewa chafu kwenye anga na kuongeza hewa safi.
Eneo la jangwani likiwa limezungukwa na maji yaliyotokana na vipindi vifupi za mvua kubwa katika msimu wa mvua za VULI 2017.

Kwa maana hiyo, kama waaminivyo wataalamu hatuna budi kufahamu kuwa kuna uhusiano mkubwa kati ya mazingira kwa maana ya uwepo wa misitu na mabadiliko ya hali ya hewa.

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), ni taasisi inayoshughulikia masuala ya hali ya hewa nchini na kuiwakilisha nchi kikanda na Kimataifa. Taasisi hii imepewa jukumu la kutoa huduma za hali ya hewa kupitia sheria ya hali ya hewa Na. 6 ya mwaka 1977. Mamlaka hii pia hutoa tahadhari ya hali mbaya ya hewa kila inapotarajiwa kuwepo na huwaelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kutumia taarifa za hali ya hewa. 

Kwa kuzingatia  matumizi sahihi ya huduma za hali ya hewa tutaweza kupunguza athari za uharibifu wa mazingira. 

TMA inasema takwimu za hali ya hewa zilizokusanywa kwa kipindi cha miongo kadhaa iliyopita zinaonesha dhahiri kuwa uharibifu wa mazingira umechangia kwa kiasi kikubwa kusababisha mabadiliko ya hali ya hewa nchini na duniani kwa ujumla.  

Mfano mkubwa wa viashirikia hivyo ni kuongezeka kwa joto na kupungua kwa mvua  katika maeneo mbalimbali nchini  kama ilivyooneshwa kwenye mwenendo wa mvua wa kitaalamu katika vielelezo vya maeneo mbalimbali nchini. 
Ongezeko la joto kwa mkoa wa Dar es salaam kuanzia mwaka 1953-2015.

Kwa vielelezo hivi, ni wazi kuwa joto limeendelea  kuongezeka miaka ya karibuni katika  mkoa wa Dar es Salaam na Kilimanjaro ukilinganisha na miaka iliyopita.
Aidha, kiwango cha mvua kinapungua kwa kiasi fulani ukilinganisha na miaka ya nyuma kama inavyoonekana kwa mkoa wa Kilimanjaro. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...