Na Khadija Seif, Globu ya Jamii.     

Michuano ya Kagame Cup 2018 yanafikia kilele chake siku ya kesho  tarehe 13 Julai  kwa kuzikutanisha Azam na Simba katika dimba la Uwanja wa Taifa.       
                                          
Katibu Mkuu wa Baraza la Vyama vya Michezo Afrika Mashariki CECAFA Nicolaus Musonye amesema  timu mbili kutoka Tanzania ambazo ni Simba na Azam zimefanikiwa kuingia fainali na zitakutana kesho ili kumfahamu Bingwa mpya wa michuano hiyo kwa mwaka 2018.

"timu zilizofanikiwa kutinga fainali ni Azam pamoja na Simba na mchezo huo utachezwa kuanzia majira ya saa 12 jioni katika Uwanja wa Taifa,"amesema Musonye

Mchuano huo utafanyika  majira ya saa 12 jioni ,huku  akiwapongeza wadau wote wa mpira Kwa kutoa michango yao kwa Hali na mali mpaka hapo walipofikia .    

Musonye ameeleza  kuwa timu 12 zote zilizoshiriki Kagame Cup zimefanya vizuri kwenye mashindano hayo na  wajitahidi, kwenye mashindano yajayo wasivunjike moyo Kwa wale wasiofanikiwa  kuingia fainali.          

Sanjari na hilo, Musonye amesema amepokea maombi kutoka nchi zingine za jirani kujiunga kwenye michuano hiyo ikiwamo Zambia,malawi pamoja na Congo .      

Musonye amewaomba  Wadau na mashabiki wa timu hizo  wajitokeze Kwa wingi na viingilio vitakuwa vya bei ya kawaida ili  watu wote waweze kumudu  kuingia japo mpaka sasa havijatangazwa rasmi alisema Musonye.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...