Na Shani Amanzi


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba Dkt.Semistatus Mashimba amewataka waandikishaji waliopata Mafunzo ya maboresho ya Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF Iliyoboreshwa) wakawatumikie vyema Wananchi kwani lengo kubwa la Serikali ni kuona jamii inapata huduma bora ya Afya. 

Dkt. Semistatus Mashimba aliyazungumza hayo alipokuwa anafungua mafunzo ya siku mbili ya Maafisa uandikishaji wa CHF wa vijiji vyote vya wilaya ya Chemba kwa kushirikiana wadau wa mradi wa HPSS-Tuimarishe afya kuanzia Tarehe 16 mpaka 17 Julai 2018 katika ukumbi wa Godown mjini Chemba. 

“Nawaomba muwe mabolozi wazuri kwa wilaya ya Chemba kwa kupunguza malalamiko na kutoa elimu ya kutosha juu ya mabadiliko ya bei ya uandikishaji wa kitambulisho cha bima ya Afya ya CHF Iliyoboreshwa kutoka tsh 13,000/= kwenda tsh 30,000/=, na lengo kubwa la serikali ni kuwasaidia wananchi hasa walio kwenye hali ya chini kupata huduma za afya katika vituo mbalimbali vya afya vilivyoko nchini” aliongeza kwa kusema hivyo Dkt.Semistatus Mashimba. 

Naye Meneja wa Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF Iliyoboreshwa) wilaya ya Chemba Ndg. Haruna Haji amesema katika zoezi la uandikishaji Wilaya ya Chemba, atahakikisha kwanza anatoa elimu ya kutosha kwa Maafisa Uandikishaji wa Mfuko wa CHF katika kila kijiji ili kuondokana na vikwazo kwa wanachama wa CHF na pia atahakikisha elimu hii muhimu ya bima ya afya inawafikia wananchi wote wilayani hapo. 

Ndg.Haji amesema “katika uhifadhi wa nyaraka kuna utunzaji mkubwa na kuendelea kuwahamasisha kukusanya fedha kamili kabla ya kutoa kitambulisho pia tunaendelea kutoa elimu kwa wananchi maboresho yanayoendelea ya CHF ikiwemo bei mpya ya kitambulisho cha CHF. 

Vilevile Afisa wa Mradi wa HPSS- Tuimarishe afya wilaya ya Chemba bi. Salome Chilongani ametoa shukurani zake kwa mkuu wa wilaya pamoja mkurugenzi wa halmashauri ya Chemba kwa kuonesha ushirikiano wao mkubwa kwenye mafunzo hayo. 

Bi. Salome amesema “Kwanza nianze kwa kutoa pongezi na shukurani kwa viongozi wetu wa wilaya ya Chemba, yaani mkuu wa wilaya pamoja na mkurugenzi wa halmashauri, kwa kuonesha ushirikiano mkubwa sana kwenye mafunzo haya, kwakweli wameshiriki kikamilifu sana na wameweza kuwaelewesha Maafisa Uandikishaji hawa umuhimu wa elimu waliyoipata na kutoa msisitizo kuilinda dhamana waliyoibeba. 

Mimi kama mdau nimefarijika kuona jinsi viongozi hawa walivyotupokea na kujali shughuli zinazotekelezwa na mradi wa HPSS, nina matumaini mwaka mmoja baada ya mafunzo haya tutafanikiwa kwa kiasi kikubwa na tutakuwa na wanachama wengi sana wa CHF katika wilaya yetu ya Chemba” 

 Mkurugenzi Mtendaji Dkt.Semistatus Mashimba akizindua Mafunzo ya CHF iliyoboreshwa

Baadhi ya Wadau mbalimbali waliohudhuria mafunzo hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...