Na WAMJW Simiyu
Wananchi wa Kijiji cha Itindilo Wilaya ya Itimilo, Nangale na Migato vilivyopo Wilaya ya Itimila mkoani Simiyu wameungana kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika kuleta maendeleo kwa kuchangia nguvu kazi zenye thamani ya Shilling Millioni 24 kujenga Zahanati na kituo cha Afya vijiji hapo.
Hayo yamebainika wakati Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile wakati akikagua huduma za Afya na Maendeleo ya Jamii katika mkoa wa Simiyu.
Taarifa ya mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Ikindilo imesema kuwa mradi huo unaogharimu jumla ya shilling 541,000,000 Shillingi 250,000,000 kutoka Serikalini, Shillingi Millioni 275,000,000 kutoka wadau wa Maendeleo UNFPA na Shillingi Millioni 16 kutokana na nguvu za wananchi.
Pia mradi ujenzi wa wodi ya Mama na Mtoto katika Zahanati ya Kijiji cha Nangale unaogharimu jumla ya shilling 36,321,000 Shillingi 30,000,000 kutoka Serikalini kwa kushirikiana na UNFPA, na Shillingi Millioni 6,321,000 kutokana na nguvu za wananchi.
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt.
Faustine Ndugulile akiweka jiwe la msingi la jengo la wodi ya mama na
mtoto ya Zahanati ya Kijiji hicho kilichopo wilaya ya Itimila mkoa wa
Simiyu.
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt.
Faustine Ndugulile akizungumza na wanakijiji wa Migato na kuwahimiza
kujitola katika kufanya shughli za kujiletea maendeleo wakati mara baada
ya kuweka jiwe la msingi la jengo la wodi ya mama na mtoto ya Zahanati
ya Kijiji hicho kilichopo wilaya ya Itimila mkoa wa Simiyu.
Wananchi wa kijiji cha magito wakisikiliza hotuba ya Naibu Waziri wa
Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine
Ndugulile( hayupo pichani) mara baada ya kuweka jiwe la msingi la jengo
la wodi ya mama na mtoto ya Zahanati ya Kijiji hicho kilichopo wilaya ya
Itimila mkoa wa Simiyu.
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt.
Faustine Ndugulile akizungumza na mtoto mkaziwa Kijiji cha Migato mara
baada ya kuweka jiwe la msingi la jengo la wodi ya mama na mtoto ya
Zahanati ya Kijiji hicho kilichopo wilaya ya Itimila mkoa wa Simiyu. Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...