Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (wa tatu kushoto), waliokaa msitari wa mbele, akifuatilia mada iliyowasilishwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Bi. Agnes Sitta Kijo (hayupo pichani).
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Bi. Agnes Sitta Kijo (wa kwanza kushoto), waliosimama, akiwasilisha mada inayohusu vigezo vya uanzishaji viwanda vya dawa nchini Tanzania kwa wadau wa kongamano la biashara la kimataifa, linalofanyikia Beijing Kempinski Hotel, Lufthansa Centre, Beijing – China.

Na Gaudensia Simwanza – Dar es Salaam
TFDA inaendelea na uhamasishaji wa wadau wa ndani na nje ya nchi katika kuanzisha viwanda vya dawa nchini Tanzania. Hivi sasa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Bi. Agnes Sitta Kijo yupo nchini China kwa ajili ya kuhamasisha wadau mbalimbali wa kimataifa kuja kufanya uwekezaji huo katika nchi yetu.

Katika mada yake aliyoiwasilisha katika kongamano la kimataifa la wadau wa dawa linalofanyikia katika Beijing Kempinski Hotel, Lufthansa Centre, Beijing – China, aliwafafanulia wadau hao kuhusu vigezo vya kisheria vinavyotakiwa na  kuwahakikishia wadau hao kwamba TFDA imeweka mazingira mazuri ya uwekezaji wa tasnia ya dawa na kwamba mwekezaji yeyote atakayekidhi vigezo hatakwamishwa bali atapewa ushirikiano kwa kuwa Tanzania ina dhamira ya dhati katika uanzishaji wa viwanda hususan vya dawa.

Matarajio ya TFDA kwa mikakati ya aina hii, ni kushuhudia uanzishwaji wa viwanda vya bidhaa zinazodhibitiwa na taasisi hii kwa nia ya kutosheleza mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi, kulinda afya ya jamii na kukuza uchumi wa nchi. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...