Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani akiongoza mkutano wa Wadau wanaohusika katika  utekelezaji wa mradi wa kuzalisha umeme katika maporomoko ya maji ya Bonde la Mto Rufiji,uliofanyika mkoani Njombe.
 Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Ussi Pondeza ( katikati), Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu( kushoto) na Kaimu Kamishna wa Umeme na Nishati Mbadala, Mhandisi Innocent Luoga (kulia) wakifuatilia mada wakati wa mkutano wa wadau wanaohusika na  utekelezaji wa mradi wa kuzalisha umeme katika maporomoko ya maji bonde la mto Rufiji, uliofanyika mkoani Njombe.
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (wa nne kulia) na Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu ( katikati mbele) wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Wizara, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini na viongozi mbalimbali kutoka mkoa wa Njombe walioshiriki mkutano wa wadau wa utekelezaji mradi wa kuzalisha umeme katika maporomoko ya maji ya bonde la mto Rufiji, uliofanyika mkoani Njombe.Kamati ya Bunge yawataka wananchi kuacha kukwamisha miradi ya maendeleo 
Na Zuena Msuya Njombe,

KAMPUNI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, imewataka wananchi kuwa wazalendo na kujali maslahi ya nchi na taifa katika kutekeleza miradi ya mikubwa ya maendeleo ukiwemo mradi kuzalisha umeme wa maji wa megawati 2100 katika maporomoko ya bonde la Mto Rufiji. 

Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Ussi Pondeza, mkoani Njombe wakati wa mkutano wa Wadau wa mradi wa kuzalisha umeme wa maji katika maporomoko ya bonde la mto Rufiji.

Pondeza alisema kuwa,  Watanzania wengi wamekuwa na tabia ya kupenda kuangalia maslahi yao binafsi kwa kutaka malipo makubwa ama fidia zinazoweza kuepukwa  pindi Serikali inapoanzisha miradi mikubwa ya maendeleo bila kujali kuwa miradi hiyo ni kwa manufaa ya Watanzania wote.

Alitoa angalizo kuwa,  tabia hiyo imekuwa ikichelewesha utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo  na hata wakati mwingine kukwamisha utekelezaji wake. 

"Baadhi yetu sisi watanzania sijui tuna tabia gani, tunaletewa mradi kwa maendeleo yetu wenyewe lakini kwa vile ni wabinafsi tunaanza kukwamisha kwa kutaka fidia ili mradi mtu upate fedha! unasahau kuwa hizo ni juhudi za Serikali katika kutuletea maendeleo sisi wenyewe,” alisema Pondeza.

Aliongeza kuwa,  kuna baadhi ya watu wakikosa huduma fulani huilalamikia Serikali kuwa haijafanya kitu hali ya kuwa wao ndio walikuwa wakizuia utekelezaji hivyo aliwataka wabadilike.
Kusoma zaidi BOFYA HAPA.                          

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...